Yobu
36 Elihu akaendelea kusema:
2 “Univumilie kidogo wakati ninaendelea kueleza,
Kwa maana ningali na maneno ya kusema kwa ajili ya Mungu.
3 Nitasema mingi juu ya mambo yenye ninajua,
Na nitamutangaza Mutengenezaji wangu kuwa mwenye haki.+
4 Kwa kweli maneno yangu hayako ya uongo;
Ule Mwenye kuwa mukamilifu katika ujuzi+ iko* hapa mbele yako.
5 Kwa kweli, Mungu ni mwenye nguvu+ na hakatae mutu yeyote;
Yeye ni mukubwa katika nguvu zake za uelewaji;*
6 Hatalinda uzima wa watu waovu,+
Lakini anapatia watu wenye kuteseka haki.+
7 Yeye haondoe macho yake juu ya watu wenye haki;+
Anawaweka juu ya viti vya ufalme pamoja na wafalme,*+ nao wanatukuzwa milele.
8 Lakini kama wamefungwa kwa pingu
Na kukamatwa katika kamba za mateso,
9 Anawafunulia mambo yenye wamefanya,
Makosa yenye walitenda kwa sababu ya kiburi chao.
10 Anafungua masikio yao ili yasikie karipio
Na anawaambia waache kutenda maovu.+
11 Kama wanatii na kumutumikia yeye,
Wataishi siku zao zote katika hali ya muzuri,
Na miaka yao itakuwa yenye kupendeza.+
13 Watu wenye hawamuogope Mungu* katika moyo wao wataweka kinyongo.
Hawalilie musaada hata wakati anawafunga.
15 Lakini Mungu* anaokoa watu wenye kuteseka katika mateso yao;
Anafungua sikio lao wakati wanakandamizwa.
16 Anakuokoa wakati unakaribia kuingia katika taabu+
Na kukupeleka mahali kwenye nafasi kubwa, kwenye hakuna kizuizi,+
Kwenye meza yenye chakula kingi kizuri ili kukufariji.+
17 Kisha utatosheka na hukumu yenye itapata watu waovu,+
Wakati hukumu itatolewa na haki kutetewa.
18 Lakini ukuwe muangalifu ili kasirani isikufanye ukuwe na chuki,*+
Na usiruhusu rushwa* kubwa ikupotoshe.
19 Je, kilio chako cha kuomba musaada
Ao bidii yako nyingi inaweza kukuzuia usipatwe na taabu?+
20 Usitamani usiku,
Wakati watu wanaangamia kutoka mahali pao.
21 Ukuwe muangalifu kwamba usigeuke ili kufanya maovu,
Kwa kuchagua maovu pahali pa mateso.+
22 Angalia! Mungu ni mwenye kuinuliwa katika nguvu zake;
Ni mufundishaji gani iko* kama yeye?
25 Wanadamu wote wameyaona,
Mwanadamu mwenye anaweza kufa ameyaangalia kwa mbali.
26 Ndiyo, Mungu ni mukubwa kuliko namna tunaweza kujua;+
27 Anakusanya juu matone ya maji;+
Yanagandamana katika kunguku yake na kufanyiza mvua;
28 Kisha mawingu yanamwanga maji hayo chini;+
Yananyesha kwa wingi juu ya wanadamu.
29 Je, mutu anaweza kuelewa namna mawingu yametandikwa,*
32 Anafunika umeme wa radi kwa mikono yake,
Na anaiongoza ili ipige shabaha yake.+
33 Mungurumo wa radi yake unaeleza habari juu yake,
Hata mifugo inaeleza mwenye anakuja.*