Zaburi
114 Wakati Israeli alitoka Misri,+
Wakati nyumba ya Yakobo ilitoka kati ya watu wenye kuzungumuza luga ya kigeni,
2 Yuda ikakuwa patakatifu* pake,
Israeli, eneo la utawala wake.+
4 Milima iliruka-ruka kama kondoo-dume,+
Vilima, kama wana-kondoo.
5 Ni nini ilikufanya ukimbie, Ee bahari?+
Sababu gani ulirudia nyuma, Ee Yordani?+
6 Sababu gani muliruka-ruka kama kondoo-dume, Enyi milima,
Kama wana-kondoo, enyi vilima?