Zaburi
Kwa kiongozi; imepatanishwa na
“Ua la Yungiyungi la Kikumbusho.” Miktamu.* Ya Daudi. Ya kufundisha. Wakati alipigana na Aram-naharaimu na Aram-Soba, na Yoabu akarudia
na akapiga na kuua Waedomu elfu
kumi na mbili (12 000) katika
Bonde la Chumvi.+
60 Ee Mungu, ulitukataa; ulipasua njia katika vikundi vyetu vya ulinzi.+
Ulitukasirikia; lakini sasa utukubali tena!
2 Ulifanya dunia itetemeke; uliipasua ikafunguka.
Funga mipasuko yake, kwa maana inaanguka.
3 Ulifanya watu wako wateseke.
Ulitufanya tukunywe divai yenye inatufanya tuyumbe-yumbe.+
4 Patia* alama wale wenye kukuogopa
Ili wakimbie na kukwepa upinde. (Sela)
5 Ili wapendwa wako waokolewe,
Utuokoe kupitia mukono wako wa kuume na utujibu.+
6 Mungu amesema katika utakatifu wake:*
7 Gileadi ni yangu, na Manase+ ni yangu,
Na Efraimu ni kofia ya chuma* ya kichwa changu;
Yuda ni fimbo yangu ya kamanda.+
8 Moabu ni beseni yangu ya kunawia.+
Nitatupa kiatu changu juu ya Edomu.+
Nitapiga vigelegele vya ushindi juu ya Ufilisti.”+
9 Ni nani atanipeleka katika muji wenye kuzungukwa kwa ajili ya vita?*
Ni nani ataniongoza mupaka Edomu?+
10 Je, haiko wewe, Ee Mungu, mwenye umetukataa,
Mungu wetu, mwenye haende tena na majeshi yetu?+
11 Utusaidie katika taabu yetu,
Kwa maana wokovu kutoka kwa wanadamu hauna mafaa yoyote.+