Zaburi
Kwa kiongozi. Ya Daudi,
ya kukumbusha.
70 Ee Mungu, uniokoe;
Ee Yehova, fanya haraka ili unisaidie.+
2 Acha wale wenye kutafuta kuondoa uzima wangu*
Wapatishwe haya na kufezeheshwa.
Acha wale wenye kufurahia musiba wangu
Wakimbie kwa sababu ya aibu.
3 Acha wale wenye kusema: “Aha! Aha!”
Wakimbizwe kwa sababu ya haya.
4 Lakini acha wale wenye kukutafuta
Wafurahi na kushangilia katika wewe.+
Acha wale wenye kupenda matendo yako ya wokovu waseme sikuzote:
“Mungu atukuzwe!”
Wewe ni musaidizi wangu na mwokozi wangu.+
Ee Yehova, usikawie.+