Zaburi
Kwa kiongozi. Imepatanishwa
na muziki wa “Usiharibu.” Ya Asafu.+ Wimbo.
75 Tunakushukuru, Ee Mungu, tunakushukuru;
Jina lako liko karibu,+
Na watu wanatangaza kazi zako za ajabu.
2 Unasema: “Wakati ninaweka muda,
Ninahukumu kwa haki.
3 Wakati dunia na wakaaji wake wote waliyeyushwa,
Mimi ndiye nilifanya nguzo zake zikuwe imara.” (Sela)
4 Ninaambia wenye kujisifu, “Musijisifu,”
Na waovu, “Musiinue nguvu zenu.*
6 Kwa maana kuinuliwa hakutoke
Mashariki wala mangaribi wala kusini.
7 Kwa maana Mungu ni Muamuzi.+
Anashusha mutu mumoja na kuinua mwingine.+
8 Kwa maana kuko kikombe katika mukono wa Yehova;+
Divai inatoa pofu na imechanganywa kwa ukamili.
9 Lakini mimi, nitatangaza hilo milele;
Nitamuimbia Mungu wa Yakobo sifa.*
10 Kwa maana anasema: “Nitakata nguvu* zote za waovu.”
Lakini nguvu* za wenye haki zitainuliwa.