Kutoka
21 “Haya ndiyo maamuzi ya hukumu yenye utawaambia:+
2 “Kama unanunua mutumwa Mwebrania,+ atafanya kazi ya utumwa kwa miaka sita (6), lakini mwaka wa saba (7), atawekwa huru bila kulipa kitu.+ 3 Kama alikuja peke yake, ataondoka peke yake. Kama iko* na bibi, basi bibi yake anapaswa kuondoka pamoja naye. 4 Kama bwana wa mutumwa huyo anamupatia bibi, na bibi huyo anamuzalia watoto wanaume ao watoto wanamuke, bibi huyo na watoto wake watakuwa mali ya bwana wa mutumwa huyo, na mutumwa huyo ataondoka peke yake.+ 5 Lakini kama mutumwa huyo anasema hivi kwa mukazo: ‘Ninamupenda bwana wangu, bibi yangu, na wana wangu; sitaki kuwekwa huru,’+ 6 bwana wa mutumwa huyo atamuleta mbele ya Mungu wa kweli. Kisha bwana huyo atamuleta kwenye mulango ao kwenye mwimo wa mulango, na bwana wa mutumwa huyo atatoboa sikio la mutumwa huyo kwa sindano, naye atakuwa mutumwa wa bwana wake maisha yake yote.
7 “Kama mutu anamuuzisha binti yake akuwe mutumwa, binti huyo hatawekwa huru kama vile mutumwa mwanaume anawekwa huru. 8 Kama bwana wa mutumwa huyo mwanamuke hamufurahie na hamuchague kuwa suria* wake lakini anamufanya anunuliwe na mutu mwingine,* bwana huyo hatakuwa na haki ya kumuuzisha kwa wageni, kwa sababu amemusaliti mutumwa huyo. 9 Kama anamuchagua akuwe bibi ya mwana wake, anapaswa kumupatia haki zenye binti yake anastahili. 10 Kama anajichukulia bibi mwingine, chakula, nguo, na haki ya ndoa ya bibi yake wa kwanza havitapunguzwa.+ 11 Kama hamupatie hayo mambo tatu (3), basi mutumwa huyo mwanamuke ataondoka na kuwa huru bila kulipa feza yoyote.
12 “Mutu yeyote mwenye anamupiga mutu na kumuua anapaswa kuuawa.+ 13 Lakini kama anamuua bila kukusudia na Mungu wa kweli anaruhusu jambo hilo litokee, nitakuchagulia mahali kwenye anaweza kukimbilia.+ 14 Kama mutu anamukasirikia sana mwenzake na kumuua kwa makusudi,+ mutu huyo anapaswa kufa hata kama inaomba kumutosha kwenye mazabahu yangu.+ 15 Mutu mwenye anamupiga baba yake ao mama yake anapaswa kuuawa.+
16 “Kama mutu yeyote anamukamata mutu mwingine kinguvu+ na kumuuzisha ao anapatikana amemushika mutu huyo,+ anapaswa kuuawa.+
17 “Mutu yeyote mwenye anamulaani baba yake ao mama yake anapaswa kuuawa.+
18 “Ni hivi mambo yatakuwa kama watu wanagombana na kama mumoja wao anamupiga mwenzake kwa jiwe ao ngumi* na hakufe lakini haweze kutoka kwenye kitanda chake: 19 Kama anaweza kusimama na kutembea inje kwa kutumia fimbo, basi ule mwenye alimupiga hatapewa azabu. Atamulipa tu kwa ajili ya wakati wenye alipoteza bila kufanya kazi mupaka akuwe amepona kabisa.
20 “Kama mutu anamupiga kwa fimbo mutumwa wake mwanaume ao mutumwa wake mwanamuke na mutumwa huyo anakufa kwa mukono wake, mutu huyo mwenye amekufa anapaswa kulipiziwa kisasi.+ 21 Lakini, kama mutumwa huyo anaendelea kuishi kwa siku moja ao siku mbili, hatalipiziwa kisasi, kwa sababu yeye ni mutu mwenye bwana wake alimununua kwa feza.
22 “Kama watu wanapigana na wanamuumiza mwanamuke mwenye mimba naye anazaa mbele ya wakati wake*+ lakini hakutokee kifo,* ule mwenye alimuumiza anapaswa kulipa amande* yenye bwana ya bibi huyo atamuomba; na anapaswa kulipa amande hiyo kupitia waamuzi.+ 23 Lakini kama kifo kinatokea, basi unapaswa kutoa uzima kwa uzima,*+ 24 jicho kwa jicho, jino kwa jino, mukono kwa mukono, muguu kwa muguu,+ 25 alama ya moto kwa alama ya moto, kidonda kwa kidonda, pigo kwa pigo.
26 “Kama mutu anapiga jicho la mutumwa wake mwanaume ao jicho la mutumwa wake mwanamuke na kuliharibu, atamuacha mutumwa huyo aende huru kwa sababu ya jicho lake.+ 27 Na kama anangoa jino la mutumwa wake mwanaume ao jino la mutumwa wake mwanamuke, atamuacha mutumwa huyo aende huru kwa sababu ya jino lake.
28 “Kama ngombe-dume anamupiga kwa pembe mwanaume ao mwanamuke na mutu huyo anakufa, ngombe-dume huyo anapaswa kupigwa majiwe mupaka akufe+ na nyama yake haitakuliwa; lakini mwenye ngombe-dume huyo hatapewa azabu. 29 Lakini kama ngombe-dume alizoea kupiga watu kwa pembe na mwenye ngombe huyo alionywa lakini hakumufunga na ngombe-dume huyo aliua mwanaume ao mwanamuke, ngombe atapigwa majiwe na mwenye ngombe-dume huyo atauawa pia. 30 Kama anaombwa kulipa ukombozi,* anapaswa kutoa kila kitu chenye ataombwa ili akomboe uzima wake.* 31 Kama ngombe-dume anamupiga kwa pembe mutoto mwanaume ao mutoto mwanamuke, mwenye ngombe-dume huyo atatendewa kulingana na uamuzi huu wa hukumu. 32 Kama ngombe-dume huyo anamupiga kwa pembe mutumwa mwanaume ao mutumwa mwanamuke, mwenye ngombe-dume huyo atamulipa bwana wa mutumwa huyo shekeli makumi tatu (30),* na ngombe huyo atapigwa majiwe mupaka akufe.
33 “Kama mutu anafunua shimo ao anachimba shimo lakini halifunike na ngombe-dume ao punda anaangukia ndani, 34 mwenye shimo hilo atalipa.+ Atamulipa mwenye munyama huyo, na munyama mwenye alikufa atakuwa wake. 35 Kama ngombe-dume wa mutu fulani anaumiza ngombe-dume wa mutu mwingine na ngombe-dume huyo anakufa, basi wanapaswa kuuzisha ngombe-dume mwenye kuwa muzima na kugawanya bei yenye ililipwa wakati aliuzishwa; na wanapaswa pia kugawanya ule munyama mwenye alikufa. 36 Lakini kama ilikuwa inajulikana kwamba ngombe-dume alikuwa anazoea kupiga kwa pembe lakini mwenye ngombe-dume huyo hakukuwa anamufunga, anapaswa kulipa ngombe-dume kwa ngombe-dume, na ngombe-dume mwenye alikufa atakuwa wake.