Kutoka
8 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Ingia kwa Farao na umuambie, ‘Yehova anasema hivi: “Ruhusu watu wangu waende ili waweze kunitumikia.+ 2 Kama unaendelea kukataa kuwaruhusu waende, nitaleta pigo la vyura katika inchi yako yote.+ 3 Na Muto Nile utajaa vyura, nao wataingia ndani ya nyumba yako, ndani ya chumba chako cha kulala, kwenye kitanda chako, ndani ya nyumba za watumishi wako na juu ya watu wako, ndani ya majiko yenu, na ndani ya vyombo vyenu vya kufinyangia unga.*+ 4 Vyura watapanda juu yako, juu ya watu wako, na juu ya watumishi wako wote.”’”
5 Kisha wakati fulani Yehova akamuambia Musa: “Ambia Haruni, ‘Nyoosha mukono wako pamoja na fimbo yako juu ya mito, mifereji ya Muto Nile, na tingitingi, na ufanye vyura wakuje juu ya inchi ya Misri.’” 6 Kwa hiyo Haruni akanyoosha mukono wake juu ya maji ya Misri, na vyura wakaanza kuja na kufunika inchi ya Misri. 7 Lakini, makuhani wenye kufanya uchawi wakafanya jambo lilelile kwa ufundi wao wa siri, na wakafanya vyura wakuje juu ya inchi ya Misri.+ 8 Kisha Farao akaita Musa na Haruni na kusema: “Mumulilie Yehova anitoshee mimi na watu wangu vyura hawa,+ kwa maana ninataka kuruhusu watu waende ili waweze kumutolea Yehova zabihu.” 9 Kisha Musa akamuambia Farao: “Ni wewe utaniambia wakati wenye ninapaswa kumulilia Mungu ili vyura watoke kwako, kwa watumishi wako, kwa watu wako, na nyumba zenu. Watabakia tu katika Muto Nile.” 10 Basi Farao akasema: “Kesho.” Kwa hiyo Musa akasema: “Itakuwa kama vile unasema ili ujue kwamba hakuna mutu mwingine mwenye kuwa kama Yehova Mungu wetu.+ 11 Vyura watatoka kwako, katika nyumba zenu, kwa watumishi wako, na kwa watu wako. Watabakia tu katika Muto Nile.”+
12 Kwa hiyo Musa na Haruni wakatoka mbele ya Farao, na Musa akamulilia Yehova kuhusu vyura wenye Mungu alikuwa ameleta juu ya Farao.+ 13 Kisha Yehova akafanya kama vile Musa alimuomba, na vyura wakaanza kufa ndani ya nyumba, viwanja, na mashamba. 14 Watu wakakusanya vyura hao marundo marundo, na inchi ikaanza kunuka. 15 Wakati Farao aliona kwamba hali imekuwa muzuri, akafanya moyo wake ukuwe mugumu,+ na akakataa kuwasikiliza, kama vile Yehova alikuwa amesema.
16 Sasa Yehova akamuambia Musa: “Ambia Haruni, ‘Nyoosha fimbo yako na upige mavumbi ya dunia, na yatakuwa imbu katika inchi yote ya Misri.’” 17 Nao wakafanya vile. Haruni akanyoosha mukono wake pamoja na fimbo yake na kupiga mavumbi ya dunia, na imbu wakakuja juu ya watu na wanyama. Mavumbi yote ya dunia yakageuka kuwa imbu katika inchi yote ya Misri.+ 18 Makuhani wenye kufanya uchawi wakajaribu kufanya jambo lilelile na kutokeza imbu kwa ufundi wao wa siri,+ lakini hawakuweza. Na imbu wakakuja juu ya watu na wanyama. 19 Kwa hiyo makuhani wenye kufanya uchawi wakamuambia Farao: “Ni kidole cha Mungu!”+ Lakini moyo wa Farao ukaendelea kuwa mugumu, na hakuwasikiliza, kama vile Yehova alikuwa amesema.
20 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Amuka asubui sana na usimame mbele ya Farao. Angalia! Anatoka ili aende kwenye maji! Na unapaswa kumuambia, ‘Yehova anasema hivi: “Ruhusu watu wangu waende ili waweze kunitumikia. 21 Lakini kama hauruhusu watu wangu waende, nitatuma mainzi* juu yako, juu ya watumishi wako, na juu ya watu na ndani ya nyumba zenu; na nyumba za Misri zitajaa mainzi, nao wataingia katika nyumba zenu; na nyumba za Misri zitajaa mainzi, na hata watafunika udongo wenye wao* wanasimama juu yake. 22 Siku hiyo nitaweka pembeni inchi ya Gosheni, mahali kwenye watu wangu wanaishi. Hakuna mainzi wenye watapatikana kule,+ na kwa jambo hilo utajua kwamba mimi, Yehova, niko katika inchi hii.+ 23 Na nitafanya kukuwe tofauti kati ya watu wangu na watu wako. Kesho alama hii itatokea.”’”
24 Na Yehova akafanya vile; na makundi makubwa ya mainzi yakaanza kushambulia nyumba ya Farao na nyumba za watumishi wake na inchi yote ya Misri.+ Inchi ikaharibiwa na mainzi hayo.+ 25 Mwishowe, Farao akaita Musa na Haruni na kusema: “Muende, mumutolee Mungu wenu zabihu katika inchi.” 26 Lakini Musa akasema: “Haiko muzuri kufanya vile, kwa sababu zabihu zenye tutamutolea Yehova Mungu wetu zitachukiza Wamisri.+ Kama tunatoa zabihu zenye kuchukiza Wamisri mbele ya macho yao, je, hawatatupiga majiwe? 27 Tutafanya safari ya siku tatu (3) katika jangwa, na kule tutamutolea Yehova Mungu wetu zabihu, kama vile alituambia.”+
28 Sasa Farao akasema: “Nitawaruhusu muende ili mumutolee Yehova Mungu wenu zabihu katika jangwa. Lakini tu, musiende mbali sana. Muniombee.”+ 29 Kisha Musa akasema: “Sasa ninatoka mbele yako, na nitamulilia Yehova, na mainzi watatoka kwa Farao, kwa watumishi wake, na kwa watu wake kesho. Lakini Farao anapaswa kuacha kutuchezea* kwa kukataa kuruhusu watu waende kumutolea Yehova zabihu.”+ 30 Basi Musa akatoka mbele ya Farao na akamulilia Yehova.+ 31 Kwa hiyo Yehova akafanya kama vile Musa alisema, na mainzi wakatoka kwa Farao, kwa watumishi wake, na kwa watu wake. Hakuna hata inzi mumoja mwenye alibakia. 32 Lakini, Farao akafanya tena moyo wake kuwa mugumu na hakuruhusu watu waende.