Isaya
12 Siku hiyo hakika utasema:
“Ninakushukuru, Ee Yehova,
Kwa maana hata kama ulinikasirikia,
Kasirani yako iliisha pole kwa pole, na ulinifariji.+
2 Angalia! Mungu ni wokovu wangu.+
Nitakuwa na tumaini na sitaogopa sana;+
Kwa maana Yah* Yehova ni nguvu zangu na uwezo wangu
Na amekuwa wokovu wangu.”+
3 Mutashota maji kwa kushangilia
Kwenye chemchemi za wokovu.+
4 Siku hiyo mutasema:
“Mumushukuru Yehova, muitie jina lake,
Mujulishe matendo yake kati ya vikundi vya watu!+
Museme kwamba jina lake limeinuliwa.+
5 Mumuimbie Yehova sifa,*+ kwa maana ametenda mambo ya ajabu.+
Jambo hilo litangazwe katika dunia yote.