Isaya
31 Ole wao wale wenye wanashuka kuenda Misri ili kutafuta musaada,+
Wenye wanategemea farasi,+
Wenye wanategemea magari ya vita kwa sababu ni mengi sana,
Na farasi wa vita* kwa sababu wako na nguvu,
Lakini hawamuangalie Mutakatifu wa Israeli,
Na hawamutafute Yehova.
Atasimama ili kushambulia nyumba ya watenda-maovu
Na ili kushambulia wale wenye wanasaidia wakosaji.+
Yehova atanyoosha mukono wake,
Kila mutu mwenye anatoa musaada atajikwaa
Na kila mutu mwenye atasaidiwa ataanguka;
Wote wataangamia wakati mumoja.
4 Kwa maana Yehova ameniambia hivi:
“Kama vile simba ananguruma, mwana-simba mwenye nguvu,* juu ya mawindo yake,
Wakati kundi lote la wachungaji linakusanywa kupigana naye,
Na haogope sauti yao
Wala kutetemeshwa na makelele yao
Ni vile pia Yehova wa majeshi atashuka ili kupigana vita
Juu ya Mulima Sayuni na juu ya kilima chake.
5 Kama ndege wenye wanashuka, ni vile Yehova wa majeshi atapigania Yerusalemu.+
Atamupigania na kumuokoa.
Atamulinda na kumukomboa.”
6 “Mumurudilie Ule mwenye mumeasi sana, Enyi watu wa Israeli.+ 7 Kwa maana siku hiyo kila mumoja atakataa miungu yake ya feza yenye haina mafaa yoyote na miungu yake ya zahabu yenye haina mafaa yoyote, yenye mikono yenu wenyewe ilitengeneza kwa zambi.
8 Na Mwashuru ataanguka kwa upanga, wenye hauko wa mwanadamu;
Na upanga, wenye hauko wa mwanadamu, utamuharibu.+
Atakimbia kwa sababu ya upanga,
Na vijana wake wanaume watafanyishwa kazi ya kulazimishwa.