Isaya
42 Angalia! Mutumishi wangu,+ mwenye ninategemeza!
Muchaguliwa wangu,+ mwenye nimekubali!*+
Ataleta haki kwa njia ya uaminifu.+
4 Hatafifia wala kupondwa mupaka wakati ataweka haki katika dunia;+
Na visiwa vitaendelea kungojea sheria yake.*
5 Mungu wa kweli, Yehova,
Muumbaji wa mbingu na Mukubwa mwenye alizitandika,+
Yeye mwenye kutandika dunia na mazao yake,+
Yeye mwenye kupatia pumuzi watu wenye kuwa juu yake,+
Na roho kwa wale wenye kutembea juu yake, anasema hivi:+
6 “Mimi, Yehova, nimekuita katika haki,
Nimeshika mukono wako.
Nitakulinda na kukutoa ukuwe agano la watu+
Na ukuwe mwangaza wa mataifa,+
7 Ili ufungue macho yenye upofu,+
Ili utoshe mufungwa katika gereza la chini ya udongo,
Na utoshe katika gereza wale wenye kukaa katika giza.+
8 Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu;
Sipatie mutu yeyote utukufu wangu,*
Wala sipatie sanamu za kuchongwa sifa yangu.+
9 Angalia, mambo ya kwanza yametokea;
Sasa ninatangaza mambo ya mupya.
Mbele yatokee, ninawaambia juu ya mambo hayo.”+
10 Mumuimbie Yehova wimbo mupya,+
Sifa yake kutoka miisho ya dunia,+
Ninyi wenye kushuka katika bahari na vyote vyenye kuijaza,
Ninyi visiwa na wakaaji wake.+
Wakaaji wa mwamba wapige vigelegele vya shangwe.
Waseme kwa sauti kubwa wakiwa kwenye kichwa cha milima.
13 Yehova atatoka kama mwanaume mwenye nguvu.+
Ataamusha bidii yake kama mupiganaji-vita.+
Atasema kwa sauti kubwa, ndiyo, atafanya makelele ya vita;
Atajionyesha kuwa mwenye nguvu kuliko maadui wake.+
14 “Nimenyamaza kwa wakati murefu.
Niliendelea kukaa kimya na kujizuia.
Kama mwanamuke mwenye kuzaa,
Nitalia kwa maumivu, nitapumua haraka-haraka, na kuishiwa pumuzi, vyote kwa wakati mumoja.
15 Nitaharibu milima na vilima,
Na nitakausha majani yake yote.
Nitageuza giza lenye kuwa mbele yao kuwa mwangaza+
Na kugeuza eneo lenye majiwe-majiwe kuwa inchi tambarare.+
Ni vile nitawafanyia, na sitawaacha.”
17 Watarudishwa na kupatishwa haya kabisa,
Wale wenye kutegemea sanamu za kuchongwa,
Wale wenye kuambia sanamu za metali:* “Ninyi ni miungu yetu.”+
19 Ni nani mwenye kuwa kipofu isipokuwa mutumishi wangu,
Mwenye kuwa kiziwi sana kama mujumbe mwenye ninatuma?
Ni nani mwenye kuwa kipofu sana kama ule mwenye alipewa zawabu,
Mwenye kuwa kipofu sana kama mutumishi wa Yehova?+
20 Unaona mambo mengi, lakini hauendelee kukaa macho.
Unafungua masikio yako, lakini hausikilize.+
21 Kwa sababu ya haki yake,
Yehova amefurahia kutukuza sheria* na kuifanya ikuwe yenye utukufu.
22 Lakini hawa ni watu wenye vitu vyao vimenyanganywa na kukamatwa kinguvu;+
Wote wamenaswa katika mashimo na kufichwa katika magereza.+
Wamenyanganywa bila mutu wa kuwaokoa,+
Na kukamatwa kinguvu bila mutu wa kusema: “Muwarudishe!”
23 Ni nani kati yenu atasikia jambo hili?
Ni nani atakaza uangalifu na kusikiliza kwa ajili ya wakati wenye utakuja?
24 Ni nani amemutoa Yakobo ili anyanganywe
Na Israeli kwa wanyanganyi?
Je, haiko Yehova, mwenye tumemutendea zambi?
Iliteketeza kila kitu kumuzunguka, lakini hakukaza uangalifu.+
Iliwaka juu yake, lakini hakukuwa anaweka jambo hilo katika moyo.+