Isaya
56 Yehova anasema hivi:
“Mushike haki,+ na mutende uadilifu,*
Kwa maana wokovu wangu utakuja hivi karibuni
Na haki yangu itafunuliwa.+
2 Mwenye furaha ni mutu mwenye anafanya jambo hili
Na mwana wa binadamu mwenye anaendelea kulishika,
Mwenye anashika Sabato na haichafue,+
Na mwenye anazuia mukono wake usitende namna yoyote ya uovu.
Na towashi hapaswe kusema, ‘Angalia! Niko muti wenye kukauka.’”
4 Kwa maana Yehova anaambia hivi matowashi wenye kushika sabato zangu na wenye kuchagua mambo yenye kunipendeza na wenye kushika agano langu:
5 “Nitawapatia munara na jina katika nyumba yangu na katika kuta zangu,
Jambo la muzuri kuliko watoto wanaume na watoto wanamuke.
Nitawapatia jina lenye kudumu,
Lenye halitaangamia.
6 Kuhusu wageni wenye kujiunga na Yehova ili kumutolea utumishi
Ili kupenda jina la Yehova+
Na kuwa watumishi wake,
Wale wote wenye kushika Sabato na hawaichafue
Na wenye kushika agano langu,
7 Pia nitawaleta kwenye mulima wangu mutakatifu+
Na kuwafanya washangilie ndani ya nyumba yangu ya sala.
Matoleo yao mazima ya kuteketezwa na zabihu zao zitakubaliwa kwenye mazabahu yangu.
Kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya vikundi vyote vya watu.”+
8 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, mwenye anakusanya wenye walisambazwa wa Israeli,+ anasema:
“Nitakusanya wengine kwake zaidi ya wale wenye tayari wamekusanywa.”+
10 Walinzi wake ni vipofu,+ hakuna hata mumoja mwenye ameona.+
Wote ni imbwa wenye kuwa bubu, hawawezi kufoka.+
Wanapumua haraka-haraka na kulala chini; wanapenda kusinzia.
Wao ni wachungaji wenye hawana uelewaji.+
Wote wamefuata njia yao wenyewe;
Kila mumoja wao anatafuta faida yenye haiko ya haki na kusema:
Na kesho itakuwa kama leo, hata muzuri zaidi!”