Yeremia
3 Watu wanauliza: “Kama mwanaume anamufukuza bibi yake na bibi huyo anamuacha na kuwa wa mwanaume mwingine, je, mwanaume huyo anapaswa kumurudilia tena?”
Je, inchi hiyo haikuchafuliwa kabisa?+
“Umefanya ukahaba na marafiki wengi,+
Na je, sasa unapaswa kurudia kwangu?” ni vile Yehova anasema.
2 “Inua macho yako kuelekea vilima vyenye kuwa wazi na uone.
Ni wapi kwenye haukulalwa kinguvu?
Ulikaa pembeni ya barabara kwa ajili yao,
Kama mutu mwenye kuhama-hama* katika jangwa;
Unaendelea kuchafua inchi
Kwa ukahaba wako na uovu wako.+
3 Kwa hiyo matone ya mvua yamezuiwa,+
Na hakuna mvua katika kipindi cha mvua ya mwisho.
Uko na uso wenye hauna haya wa* bibi mwenye anafanya ukahaba.
Unakataa kusikia haya.+
4 Lakini sasa unaniita ukisema,
‘Baba yangu, wewe ni rafiki wa ujana wangu!+
5 Je, mutu anapaswa kuendelea kuwa na kinyongo milele,
Ao kuwa na uchungu sikuzote?’
Ni vile unasema,
Lakini unaendelea kufanya mambo yote maovu yenye unaweza kufanya.”+
6 Katika siku za mufalme Yosia,+ Yehova aliniambia: “‘Je, umeona jambo lenye Israeli mwenye kukosa uaminifu amefanya? Ameenda juu ya kila mulima murefu na chini ya kila muti wenye majani mengi ili afanye ukahaba.+ 7 Hata kisha kufanya mambo hayo yote, niliendelea kumuambia arudie kwangu,+ lakini hakurudia; na Yuda akaendelea kumuangalia dada yake mudanganyifu.+ 8 Wakati niliona vile, nikafukuza Israeli mwenye kukosa uaminifu akiwa na cheti kamili cha kuvunja ndoa+ kwa sababu ya uzinifu wake.+ Lakini Yuda dada yake mudanganyifu hakuogopa; yeye pia alienda na kufanya ukahaba.+ 9 Aliona ukahaba wake kuwa jambo la kidogo, na akaendelea kuchafua inchi na kufanya uzinifu na majiwe na miti.+ 10 Ijapokuwa mambo hayo yote, Yuda dada yake mudanganyifu hakurudia kwangu kwa moyo wake wote, lakini kwa unafiki tu,’ ni vile Yehova anasema.”
11 Kisha Yehova akaniambia: “Israeli mwenye kukosa uaminifu amejionyesha kuwa mwenye* haki kuliko Yuda mudanganyifu.+ 12 Uende na utangaze maneno haya upande wa kaskazini:+
“‘“Rudia, Ee Israeli mwenye kuasi,” ni vile Yehova anasema.’+ ‘“Sitakuangalia kwa kasirani,*+ kwa maana mimi ni mushikamanifu,” ni vile Yehova anasema.’ ‘“Sitaendelea kuwa na kinyongo milele. 13 Isipokuwa tu ukubali hatia yako, kwa maana umemuasi Yehova Mungu wako. Uliendelea kutawanya wema wako* kwa wageni* chini ya kila muti wenye majani mengi, lakini haukutii sauti yangu,” ni vile Yehova anasema.’”
14 “Murudie, ninyi wana waasi,” ni vile Yehova anasema. “Kwa maana nimekuwa bwana wenu* wa kweli; na nitawakamata ninyi, mumoja kutoka katika muji mumoja na wawili kutoka katika familia moja, na nitawaleta Sayuni.+ 15 Na nitawapatia ninyi wachungaji kulingana na moyo wangu mwenyewe,+ na watawakulisha ninyi kwa ujuzi na ufahamu. 16 Mutakuwa wengi na mutazaa matunda katika inchi katika siku hizo,” ni vile Yehova anasema.+ “Hawatasema tena, ‘Sanduku la agano la Yehova!’ Halitaingia katika moyo, na hawatalikumbuka ao kulitamani, na halitafanywa tena. 17 Wakati huo wataita Yerusalemu kiti cha ufalme cha Yehova;+ na mataifa yote yatakusanywa pamoja kwa jina la Yehova katika Yerusalemu,+ na hawatafuata kwa kichwa-nguvu moyo wao muovu.”
18 “Katika siku hizo watatembea pamoja, nyumba ya Yuda pembeni ya nyumba ya Israeli,+ na pamoja watatoka katika inchi ya kaskazini na kuingia katika inchi yenye nilipatia mababu zenu kuwa uriti.+ 19 Na nilifikiri, ‘Namna nilikuweka kati ya wana na kukupatia inchi yenye kutamanika, uriti muzuri zaidi kati ya mataifa!’*+ Pia nilifikiri mutaniita, ‘Baba yangu!’ na kwamba hamutageuka na kuacha kunifuata. 20 ‘Kwa kweli kama vile bibi anamuacha bwana yake* kwa udanganyifu, ni vile ninyi pia, Ee nyumba ya Israeli, mumenitendea kwa udanganyifu,’+ ni vile Yehova anasema.”
21 Sauti inasikika kwenye vilima vyenye kuwa wazi,
Kulia na kusihi kwa watu wa Israeli,
Kwa maana wamepotosha njia yao;
Wamemusahau Yehova Mungu wao.+
22 “Murudie, ninyi wana waasi.
Nitaponyesha hali yenu ya uasi.”+
“Sisi hawa! Tumekuja kwako,
Kwa maana wewe, Ee Yehova, ni Mungu wetu.+
23 Kwa kweli vilima na muvurugo juu ya milima ni udanganyifu.+
Kwa kweli wokovu wa Israeli uko katika Yehova Mungu wetu.+