Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 34
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Yeremia

      • Ujumbe wa hukumu kwa Sedekia (1-7)

      • Agano la kuachilia huru watumwa linavunjwa (8-22)

Yeremia 34:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 25:1; Yer 32:2; 39:1; 52:4

Yeremia 34:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 36:11; Yer 37:1
  • +Yer 21:10; 32:28, 29; 39:8

Yeremia 34:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 37:17; 39:5
  • +2 Fal. 25:6, 7; Eze 12:13

Yeremia 34:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 17:16

Yeremia 34:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 4:5
  • +Mik 1:13
  • +Yosh. 15:20, 35

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    15/11/2007, uku. 14

Yeremia 34:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 21:2

Yeremia 34:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 24:7
  • +Kut 13:3

Yeremia 34:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 21:2; Law. 25:10, 39-42; Kum 15:12

Yeremia 34:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “leo.”

Yeremia 34:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kama vile nafsi yao ilitaka.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 19:12

Yeremia 34:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 21:2; Law. 25:10
  • +2 Fal. 25:3; Yer 21:7
  • +Yer 15:2, 4; 29:18

Yeremia 34:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 15:10, 17

Yeremia 34:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wenye wanatafuta nafsi zao.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 28:26; Zab 79:2; Yer 16:4

Yeremia 34:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wenye wanatafuta nafsi zao.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 25:6, 7; Omb 4:20
  • +Yer 37:5

Yeremia 34:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 25:9, 10; Yer 32:29; 39:8
  • +Law. 26:33; Yer 44:2

Maandiko ingine

Yer. 34:12 Fal. 25:1; Yer 32:2; 39:1; 52:4
Yer. 34:22Nya 36:11; Yer 37:1
Yer. 34:2Yer 21:10; 32:28, 29; 39:8
Yer. 34:3Yer 37:17; 39:5
Yer. 34:32 Fal. 25:6, 7; Eze 12:13
Yer. 34:5Eze 17:16
Yer. 34:7Yer 4:5
Yer. 34:7Mik 1:13
Yer. 34:7Yosh. 15:20, 35
Yer. 34:8Kut 21:2
Yer. 34:13Kut 24:7
Yer. 34:13Kut 13:3
Yer. 34:14Kut 21:2; Law. 25:10, 39-42; Kum 15:12
Yer. 34:16Law. 19:12
Yer. 34:17Kut 21:2; Law. 25:10
Yer. 34:172 Fal. 25:3; Yer 21:7
Yer. 34:17Yer 15:2, 4; 29:18
Yer. 34:18Mwa 15:10, 17
Yer. 34:20Kum 28:26; Zab 79:2; Yer 16:4
Yer. 34:212 Fal. 25:6, 7; Omb 4:20
Yer. 34:21Yer 37:5
Yer. 34:222 Fal. 25:9, 10; Yer 32:29; 39:8
Yer. 34:22Law. 26:33; Yer 44:2
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Yeremia 34:1-22

Yeremia

34 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova, wakati Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni na jeshi lake lote na falme zote za dunia zenye kuwa chini ya mamlaka yake na watu wote walikuwa wanapigana vita juu ya Yerusalemu na miji yake yote:+

2 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Uende na useme na Mufalme Sedekia+ wa Yuda na umuambie: “Yehova anasema hivi: ‘Angalia, ninatia muji huu katika mukono wa mufalme wa Babiloni, na atauteketeza kwa moto.+ 3 Na hautaponyoka kutoka katika mukono wake, kwa maana hakika utakamatwa na kutiwa katika mukono wake.+ Na utamuona Mufalme wa Babiloni macho kwa macho, na atasema na wewe uso kwa uso, na utaenda Babiloni.’+ 4 Hata hivyo, sikia neno la Yehova, Ee Mufalme Sedekia wa Yuda, ‘Yehova anasema hivi juu yako wewe: “Hautakufa kwa upanga. 5 Utakufa kwa amani,+ na watakufanyia sikukuu ya kuchoma manukato kama vile walifanyia baba zako, wafalme wa zamani wenye walikutangulia, na watakuombolezea, ‘Aa, Ee bwana!’ kwa maana ‘nimesema neno hilo,’ ni vile Yehova anasema.”’”’”

6 Kisha Yeremia nabii akamuambia maneno haya yote Mufalme Sedekia wa Yuda katika Yerusalemu, 7 wakati majeshi ya mufalme wa Babiloni yalikuwa yanapiga vita juu ya Yerusalemu na juu ya miji yote ya Yuda yenye ilibakia,+ juu ya Lakishi+ na juu ya Azeka;+ kwa maana hiyo ndiyo tu ilikuwa miji yenye ngome yenye ilibakia kati ya miji ya Yuda.

8 Neno lenye lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova kisha Mufalme Sedekia kufanya agano pamoja na watu wote wenye walikuwa katika Yerusalemu ili kuwatangazia uhuru,+ 9 kwamba kila mutu aachilie huru watumwa wake Waebrania, wanaume na wanamuke, ili mutu yeyote asiendelee kumufanya Muyahudi mwenzake kuwa mutumwa wake. 10 Basi wakubwa wote na watu wote wakatii. Walikuwa wameingia katika agano kwamba kila mutu aachilie huru watumwa wake wanaume na wanamuke na asiendelee tena kuwafanya kuwa watumwa. Wakatii na wakawaacha waende. 11 Hata hivyo, kisha wakati fulani walirudisha watumwa wao wanaume na wanamuke wenye walikuwa wameachilia huru, na wakawalazimisha kurudia katika utumwa. 12 Basi neno la Yehova likakuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova, na kusema:

13 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Nilifanya agano pamoja na mababu zenu+ katika siku yenye niliwatosha katika inchi ya Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa,+ nikisema: 14 “Kwenye mwisho wa miaka saba (7), kila mumoja wenu anapaswa kumuachilia huru ndugu yake Mwebrania mwenye aliuzishwa kwako na amekutumikia miaka sita (6); unapaswa kumuachilia huru.”+ Lakini mababu zenu hawakunisikiliza wala kunitegea masikio yao. 15 Na hivi karibuni* ninyi wenyewe muligeuka na kufanya mambo yenye kuwa sawa mbele ya macho yangu kwa kutangazia wenzenu uhuru, na mukafanya agano mbele yangu katika nyumba yenye kubeba jina langu. 16 Lakini kisha, muligeuka na kuchafua jina langu+ kwa kurudisha watumwa wenu wanaume na wanamuke wenye mulikuwa mumeachilia huru kama vile walitaka,* na mukawalazimisha kurudia katika utumwa.’

17 “Kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘Hamukunitii katika kutangaza uhuru, kila mutu kwa ndugu yake na kwa mwenzake.+ Basi sasa nitawatangazia ninyi uhuru,’ ni vile Yehova anasema, ‘kwa upanga, ugonjwa wa kuambukiza, na njaa,+ na nitawafanya ninyi kuwa kitu cha kuogopesha kwa falme zote za dunia.+ 18 Na ni hivi itafanyika kwa watu wenye walivunja agano langu kwa kukosa kutenda maneno ya agano lenye walifanya mbele yangu wakati walikata kitoto-dume cha ngombe vipande mbili na kupita katikati ya vile vipande,+ 19 ni kusema, wakubwa wa Yuda, wakubwa wa Yerusalemu, maofisa wa makao ya mufalme, makuhani, na watu wote wa inchi wenye walipita katikati ya vile vipande vya kitoto-dume cha ngombe: 20 Nitawatia katika mukono wa maadui wao na katika mukono wa wale wenye wanatafuta kuondoa uzima wao,* na maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa mbinguni na cha wanyama wa dunia.+ 21 Na nitatia Mufalme Sedekia wa Yuda na wakubwa wake katika mukono wa maadui wao na katika mukono wa wale wenye wanatafuta kuondoa uzima wao* na katika mukono wa majeshi ya mufalme wa Babiloni,+ yenye yanaondoka kuwaacha ninyi.’+

22 “‘Angalia, nitatoa agizo,’ ni vile Yehova anasema, ‘na nitawarudisha katika muji huu, na wataupiga vita na kuukamata na kuuteketeza kwa moto;+ na nitafanya miji ya Yuda kuwa eneo lenye limeachwa, bila mukaaji.’”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine