Yeremia
6 Mukimbilie mahali kwenye usalama, Enyi wana wa Benyamini, mbali na Yerusalemu.
Kwa maana musiba unaangalia kutoka kaskazini, musiba mukubwa.+
2 Binti ya Sayuni anafanana na mwanamuke mwenye sura na umbo ya muzuri na mwenye kuwa teketeke.+
3 Wachungaji na makundi yao watakuja.
Watasimamisha mahema yao kumuzunguka pande zote,+
Kila mumoja akikulisha kundi lenye liko chini ya ulinzi wake.+
4 “Mujitayarishe ili kupigana naye vita!*
Musimame, na tumushambulie katikati ya muchana!”
“Ole wetu, kwa maana muchana unaisha,
Kwa maana vivuli vya mangaribi vinakuwa vya murefu zaidi!”
5 “Musimame, na tumushambulie usiku
Na kuharibu minara yake yenye ngome.”+
6 Kwa maana Yehova wa majeshi anasema hivi:
“Mukate miti na mujenge boma la kuzunguka Yerusalemu kwa ajili ya vita.+
Yeye ni muji wenye unapaswa kuombwa utoe hesabu;
Ndani yake muko ukandamizaji tu.+
7 Kama vile tangi linalinda maji yake yakiwa baridi,
Ni vile anaweka uovu wake ukiwa baridi.
Jeuri na uharibifu vinasikiwa ndani yake;+
Ugonjwa na pigo viko mbele yangu sikuzote.
8 Upewe onyo, Ee Yerusalemu, ao nitageuka na kukuacha* nikiwa nimechukizwa;+
Nitakufanya ukuwe ukiwa, inchi yenye haina wakaaji.”+
9 Yehova wa majeshi anasema hivi:
“Wataokota kwa ukamili mabaki ya Israeli kama zabibu za mwisho kwenye muzabibu.
Pitisha mukono wako tena kama mutu mwenye kukusanya zabibu kwenye mizabibu.”
10 “Nitasema na nani na kumupatia onyo?
Ni nani mwenye atasikiliza?
Angalia! Masikio yao yamefungwa,* na hivyo hawawezi kusikiliza.+
Angalia! Neno la Yehova limekuwa kitu chenye wanazarau,+
Hawapendezwe nalo.
11 Basi nimejaa kasirani kali ya Yehova,
Na nimechoka kuibeba.”+
“Uimwange juu ya mutoto katika barabara,+
Juu ya vikundi vya vijana wenye kukusanyika pamoja.
12 Nyumba zao zitapewa watu wengine,
Pamoja na mashamba yao na bibi zao.+
Kwa maana nitanyoosha mukono wangu juu ya wakaaji wa inchi,” ni vile Yehova anasema.
13 “Kwa maana kuanzia mudogo zaidi mupaka mukubwa zaidi, kila mumoja anajipatia faida yenye haiko ya haki;+
Kuanzia nabii mupaka kuhani, kila mumoja anatenda kwa upunjaji.+
14 Na wanajaribu kuponyesha kijuujuu kuvunjika kwa watu wangu, wakisema,
‘Kuko amani! Kuko amani!’
Wakati hakuna amani.+
15 Je, wanasikia haya kwa sababu ya mambo yenye kuchukiza yenye wamefanya?
Hawasikie haya hata kidogo!
Hata hawajue namna ya kufezeheka!+
Basi wataanguka kati ya wale wenye kuanguka.
Wakati nitaleta azabu juu yao watajikwaa,” ni vile Yehova anasema.
16 Yehova anasema hivi:
“Musimame kwenye makutano ya barabara na muone.
Muulize juu ya barabara za zamani,
Muulize njia ya muzuri iko wapi, na mutembee ndani yake,+
Na mupate pumuziko kwa ajili yenu wenyewe.”*
Lakini wanasema: “Hatutatembea ndani yake.”+
Lakini wakasema: “Hatutasikiliza.”+
18 “Kwa hiyo musikie, Enyi mataifa!
Na mujue, Ee mukusanyiko,
Jambo lenye litawapata wao.
19 Sikiliza, Ee dunia!
Ninaleta musiba juu ya watu hawa+
Kama matunda ya mipango yao wenyewe,
Kwa maana hawakusikiliza maneno yangu
Na walikataa sheria yangu.”*
Matoleo yenu mazima ya kuteketezwa hayakubalike,
Na zabihu zenu hazinipendeze.”+
21 Kwa hiyo Yehova anasema hivi:
“Angalia, ninawekea watu hawa vikwazo,
Na watajikwaa juu yake,
Baba na wana pamoja,
Jirani na mwenzake,
Na wote wataangamia.”+
22 Yehova anasema hivi:
“Angalia! Watu wanakuja kutoka inchi ya kaskazini,
Na taifa kubwa litaamushwa kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+
23 Watashika upinde na mukuki mudogo.
Hawana huruma na hawatakuwa na rehema.
Sauti yao itanguruma kama bahari,
Na wanapanda juu ya farasi.+
Wanajipanga katika utaratibu wa vita kama mwanaume wa vita juu yako, Ee binti ya Sayuni.”
24 Tumesikia habari zake.
25 Usiende katika eneo la mashamba,
Na usitembee katika barabara,
Kwa maana adui iko* na upanga;
Kuko woga kuzunguka pande zote.
26 Ee binti ya watu wangu,
Vaa nguo ya gunia+ na ujizungushe katika majivu.
Omboleza kama vile unamuombolezea mwana wa pekee, kwa kilio cha uchungu,+
Kwa maana mwenye kuharibu atakuja juu yetu kwa kushitukia.+
27 “Nimekufanya wewe* kuwa mupimaji wa metali kati ya watu wangu,
Mutu mwenye kufanya uchunguzi kamili;
Unapaswa kuangalia na kuchunguza njia yao.
Wako kama shaba na chuma;
Wote wamepotoka.
29 Vyombo vya kuingiza upepo katika tanuru ya moto vimeunguzwa.*
Risasi inatoka ndani ya moto wao.
30 Feza yenye kukataliwa ni vile hakika watu watawaita,
Kwa maana Yehova amewakataa.”+