Ezekieli
19 “Unapaswa kuimba wimbo wa huzuni* kuhusu wakubwa wa Israeli, 2 na kusema,
‘Mama yako alikuwa nani? Simba-dike kati ya simba.
Alilala kati ya wana-simba wenye nguvu* naye akalea vitoto vyake.
3 Alilea mumoja wa vitoto vyake, akakuwa mwana-simba mwenye nguvu.+
Akajifunza namna ya kupasua mawindo,
Akapasua vipande-vipande hata wanadamu.
4 Mataifa yalisikia kumuhusu na wakamukamata katika shimo lao,
5 Mama huyo alingojea na mwishowe akaona kwamba hakuna tumaini la kurudia kwa kitoto hicho.
Basi akamukamata mwingine kati ya vitoto vyake na kumutuma akiwa mwana-simba mwenye nguvu.
6 Naye pia alitembea huku na huku kati ya simba na akakuwa mwana-simba mwenye nguvu.
Akajifunza namna ya kupasua mawindo, na akapasua vipande-vipande hata wanadamu.+
7 Akatembea kwa kuvizia-vizia kati ya minara yao yenye ngome na kuharibu miji yao,
Na hivyo inchi yenye kuwa ukiwa ikajaa sauti ya mungurumo wake.+
8 Mataifa ya wilaya zenye kumuzunguka wakakuja kumushambulia ili kutupa wavu wao* juu yake,
Naye akakamatwa katika shimo lao.
9 Wakamutia katika kizimba* kwa kulabu* na kumuleta kwa mufalme wa Babiloni.
Wakamufunga kule ili sauti yake isisikiwe tena katika milima ya Israeli.
10 Mama yako alikuwa kama muzabibu+ katika damu yako,* wenye ulipandwa pembeni ya maji.
Ukazaa matunda na ukajaa matawi kwa sababu ya maji mengi.
11 Ukatokeza matawi yenye* nguvu, yenye kustahili kuwa fimbo za ufalme za watawala.
Ukakomaa na kuwa murefu kuliko miti ingine,
Nao ukaonekana kwa sababu ya urefu wake na kwa sababu ya wingi wa majani yake.
12 Lakini alingolewa kwa kasirani kali+ na kutupwa chini,
Na upepo wa mashariki ukakausha matunda yake.
Matawi yake yenye nguvu yalikatwa na kukauka,+ na moto ukayateketeza.+
13 Sasa amepandwa katika jangwa,
Katika inchi yenye haina maji na yenye kiu.+
14 Moto ukaenea kutoka katika matawi* yake na kuteketeza machipukizi yake na matunda yake,
Na hakuna tawi lenye nguvu lenye lilibakia, hakuna fimbo ya ufalme ya kutawala.+
“‘Huo ni wimbo wa huzuni, na utatumiwa kama wimbo wa huzuni.’”