Ezekieli
23 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, kulikuwa wanamuke wawili wenye walikuwa mabinti wa mama mumoja.+ 3 Wakakuwa makahaba kule Misri;+ tangu ujana wao walifanya ukahaba. Maziwa yao yalifinywa-finywa kule, na vifua vyao vya ubikira vilipapaswa-papaswa. 4 Majina yao yalikuwa Ohola,* ule mukubwa, na Oholiba* dada yake. Wakakuwa wangu na wakazaa watoto wanaume na watoto wanamuke. Kuhusu majina yao, Ohola ni Samaria,+ na Oholiba ni Yerusalemu.
5 “Ohola akaanza kufanya ukahaba+ wakati alikuwa wangu. Alitamani sana wale wenye walimupenda kwa tamaa,+ majirani wake Waashuru.+ 6 Walikuwa magavana wenye kuvaa nguo za rangi ya bluu na watawala-wasaidizi—wote walikuwa vijana wenye kupendeza wenye walipanda farasi zao. 7 Akaendelea kufanya ukahaba na wana wote wazuri sana wa Ashuru, na akajichafua+ kupitia sanamu zenye kuchukiza* za wale wenye alitamani sana. 8 Hakuacha ukahaba wenye alizoea kufanya kule Misri, kwa maana katika ujana wake walilala naye, nao walipapasa-papasa kifua chake cha ubikira na kumwanga tamaa yao kubwa ya ngono* juu yake.+ 9 Kwa hiyo nikamutia katika mukono wa wale wenye walimupenda kwa tamaa, wana wa Ashuru,+ wenye alitamani sana. 10 Walifunua uchi wake+ na kukamata watoto wake wanaume na watoto wake wanamuke,+ nao wakamuua kwa upanga. Akakuwa na sifa mubaya kati ya wanamuke, nao wakaleta hukumu juu yake.
11 “Wakati dada yake Oholiba aliona jambo hilo, tamaa yake kubwa ya ngono ikakuwa ya mubaya zaidi, na ukahaba wake ukakuwa mubaya kuliko wa dada yake.+ 12 Alitamani sana majirani wake wana wa Ashuru,+ magavana na watawala-wasaidizi wenye walikuwa wamevaa utukufu na wenye walikuwa wamepanda farasi—wote walikuwa vijana wenye kupendeza. 13 Wakati alijichafua, niliona kwamba wote wawili walikuwa wamefuata njia ileile.+ 14 Lakini aliendelea kuongeza kwenye matendo yake ya ukahaba. Aliona wanaume wenye walikuwa wamechongwa katika ukuta, sanamu za Wakaldayo zenye zilichongwa na kupakwa rangi nyekundu sana, 15 wakiwa wamevaa mikaba* kuzunguka viuno vyao, na vilemba vyenye kuninginia kwenye vichwa vyao, wakiwa na sura ya wapiganaji-vita, wote wakionyesha Wababiloni, wenye walizaliwa katika inchi ya Wakaldayo. 16 Akaanza kusikia tamaa kubwa ya kufanya nao ngono wakati tu aliwaona, naye akatuma wajumbe kwao kule Ukaldayo.+ 17 Kwa hiyo wana wa Babiloni wakaendelea kuja kwenye kitanda chake cha mapenzi, nao wakamuchafua kwa tamaa yao kubwa ya ngono.* Kisha kuchafuliwa nao, akawaacha* akiwa amechukizwa.
18 “Wakati aliendelea kufanya ukahaba bila haya na kufunua uchi wake,+ nilimuacha nikiwa nimechukizwa, kama vile mimi nilimuacha* dada yake nikiwa nimechukizwa.+ 19 Naye akaendelea kuongeza matendo yake ya ukahaba,+ akikumbuka siku za ujana wake wakati alifanya ukahaba katika inchi ya Misri.+ 20 Aliwatamani sana kama masuria* wa wanaume wenye viungo vyao vya kiume viko kama viungo vya kiume vya punda na wenye viungo vyao vya uzazi viko kama vya farasi. 21 Ulitamani sana mwenendo muchafu wa ujana wako kule Misri+ wakati walipapasa-papasa kifua chako, maziwa ya ujana wako.+
22 “Kwa hiyo, Oholiba, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Angalia, ninachochea wale wenye walikupenda+ wenye wewe uliacha ukiwa umechukizwa,* na nitawaleta wakushambulie kutoka kila upande,+ 23 wana wa Babiloni+ na Wakaldayo wote,+ watu wa Pekodi+ na Shoa na Koa, pamoja na wana wote wa Ashuru. Wote ni vijana wenye kupendeza, magavana na watawala-wasaidizi, wapiganaji-vita wenye walichaguliwa,* wote wamepanda farasi. 24 Watakushambulia kwa makelele ya magari ya vita na magurudumu* pamoja na mukusanyiko mukubwa wa wanajeshi, pamoja na ngao ya mukubwa na ngao ya kidogo* na kofia ya chuma. Watajipanga kukuzunguka pande zote, na nitawaruhusu wafanye hukumu, nao watakuhukumu namna wataona inastahili.+ 25 Nitaleta gazabu yangu juu yako, nao watakutendea kwa kasirani kali. Watakata pua yako na masikio yako, na watu wako wenye watabakia wataanguka kwa upanga. Watabeba watoto wako wanaume na watoto wako wanamuke, na watu wako wenye watabakia watateketezwa kwa moto.+ 26 Watakuvua nguo zako+ na kunyanganya vitu vyako vya muzuri vya kujipamba.*+ 27 Nitakomesha mwenendo wako muchafu na ukahaba wako,+ wenye ulianzia katika inchi ya Misri.+ Utaacha kuwaangalia, na hautakumbuka Misri tena.’
28 “Kwa maana Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Angalia, niko karibu kukutia katika mukono wa wale wenye unachukia, wale wenye uliacha* ukiwa umechukizwa.+ 29 Watakutendea kwa chuki na kubeba kila kitu chenye ulifanyia kazi kwa jasho+ na kukuacha ukiwa uchi na mwili wazi. Uchi wenye kuleta haya wa uasherati wako na mwenendo wako muchafu na ukahaba wako vitafunuliwa.+ 30 Utafanyiwa mambo hayo kwa sababu ulifuatilia mataifa kama vile kahaba,+ kwa sababu ulijichafua kwa sanamu zao zenye kuchukiza.+ 31 Umefuata njia ileile yenye dada yako alifuata,+ na nitatia kikombe chake katika mukono wako.’+
32 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:
‘Utakunywa kikombe kirefu na kipana cha dada yako,+
Na utakuwa kitu cha kuchekwa na kuzihakiwa, na kikombe hicho kiko ndani mambo mengi.+
33 Utalemewa na* ulevi na huzuni,
Kikombe cha woga mukubwa na uharibifu,
Kikombe cha dada yako, Samaria.
34 Utalazimika kukikunywa na kukimaliza kabisa+ na kutafuna vipande vyake vya udongo,
Kisha utangoa maziwa yako.
“Kwa maana mimi mwenyewe nimesema,” ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.’
35 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu umenisahau na umenizarau kabisa,*+ utapata matokeo ya mwenendo wako muchafu na matendo yako ya ukahaba.’”
36 Kisha Yehova akaniambia: “Mwana wa binadamu, je, utatangaza hukumu juu ya Ohola na Oholiba+ na uwaambie waziwazi matendo yao yenye kuchukiza? 37 Wamefanya uzinifu,*+ na damu iko kwenye mikono yao. Haiko uzinifu tu ndio wamefanya pamoja na sanamu zao zenye kuchukiza, lakini pia wamepitisha wana wao wenye walinizalia katika moto ili wakuwe chakula cha sanamu zao.+ 38 Tena, hili ndilo jambo lenye wamenifanyia: Walichafua patakatifu pangu katika siku hiyo, na walichafua sabato zangu. 39 Wakati walimaliza kuchinja wana wao ili wakuwe zabihu kwa sanamu zao zenye kuchukiza,+ waliingia patakatifu pangu ili kupachafua+ siku hiyohiyo. Ni vile walifanya ndani ya nyumba yangu mwenyewe. 40 Hata walimutuma mujumbe ili wanaume wakuje kutoka mbali.+ Wakati walikuwa wanakuja, ulioga na kupakaa rangi kwenye macho yako na kujipamba kwa mapambo.+ 41 Na ukakaa kwenye kitanda kizuri sana+ na meza iliwekwa mbele ya kitanda hicho,+ yenye juu yake ulitia uvumba wangu+ na mafuta yangu.+ 42 Sauti ya watu wengi wenye hawana mahangaiko ilisikika kule, na kati yao kulikuwa walevi wenye waliletwa kutoka katika jangwa. Walitia vikomo kwenye mikono ya wanamuke na mataji ya muzuri kwenye vichwa vyao.
43 “Basi nikasema kuhusu ule mwenye uzinifu umemufanya achuye: ‘Sasa ataendelea kufanya ukahaba wake.’ 44 Kwa hiyo wakaendelea kuingia kwake, kama vile mutu anaenda kwa kahaba. Ni vile walienda kwa Ohola na kwa Oholiba, wanamuke wenye mwenendo muchafu. 45 Lakini wenye haki watamuhukumu kwa hukumu yenye inastahili uzinifu+ na umwangaji wa damu;+ kwa maana wao ni wazinifu na wako na damu kwenye mikono yao.+
46 “Kwa maana Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Jeshi litaletwa juu yao ili kuwafanya kuwa kitu cha kuogopesha sana na kitu cha kunyanganywa.+ 47 Jeshi hilo litawatupia majiwe+ na kuwakata kwa panga zao. Wataua watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke+ na kuteketeza nyumba zao kwa moto.+ 48 Nitakomesha mwenendo muchafu katika inchi, na wanamuke wote watajifunza somo na hawataiga mwenendo wenu muchafu.+ 49 Wataleta juu yenu matokeo ya mwenendo wenu muchafu na ya zambi zenu pamoja na sanamu zenu zenye kuchukiza; na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova.’”+