Ezekieli
25 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, elekeza uso wako kwa Waamoni,+ na utoe unabii juu yao.+ 3 Unapaswa kusema kuhusu Waamoni, ‘Musikie neno la Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova. Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Kwa sababu ulisema ‘Aha!’ juu ya patakatifu pangu wakati palichafuliwa, na juu ya inchi ya Israeli wakati iliachwa ukiwa, na juu ya nyumba ya Yuda wakati walienda katika uhamisho, 4 kwa hiyo, ninakutia katika mukono wa watu wa Mashariki ili ukuwe mali yao. Watasimamisha kambi zao* ndani yako na kusimamisha mahema yao kati yako. Watakula matunda yako, na kunywa maziwa yako. 5 Nitafanya Raba+ kuwa eneo la malisho kwa ajili ya ngamia, na inchi ya Waamoni kuwa mahali pa kupumuzikia kwa ajili ya kundi; na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”’”
6 “Kwa maana Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu ulipiga mikono+ na kupiga vishindo kwa miguu yako na ulishangilia* juu ya inchi ya Israeli kwa zarau kamili kama hiyo,+ 7 kwa hiyo nitanyoosha mukono wangu juu yako ili kukutia katika mukono wa mataifa kusudi ukuwe kitu cha kunyanganywa. Nitakuondoa katikati ya vikundi vya watu na kukuharibu kutoka katika inchi hizo.+ Nitakuharibu, na utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’
8 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu Moabu+ na Seiri+ wamesema, “Angalia! Nyumba ya Yuda iko kama mataifa mengine yote,” 9 ninaacha wazi upande* wa Moabu kwenye miji yake yenye kuwa kwenye mupaka wake, uzuri wa* inchi yake, Bet-yeshimoti, Baal-meoni, na kufikia Kiriataimu,+ 10 nitaitoa pamoja na Waamoni kuwa mali ya watu wa Mashariki,+ ili Waamoni wasikumbukwe kati ya mataifa.+ 11 Na nitafanya hukumu katika Moabu,+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’
12 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Edomu amelipiza kisasi juu ya nyumba ya Yuda na amekuwa na hatia kubwa kwa kulipiza kisasi juu yao;+ 13 kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Pia nitanyoosha mukono wangu juu ya Edomu na kuondoa ndani yake mwanadamu na mifugo, na nitafanya ikuwe ukiwa.+ Kuanzia Temani mupaka Dedani, wataanguka kwa upanga.+ 14 ‘Nitalipiza kisasi juu ya Edomu kwa mukono wa watu wangu Israeli.+ Wataleta hasira yangu na kasirani yangu kali juu ya Edomu, ili wapatwe na kisasi changu mwenyewe,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”’
15 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu ya chuki yao yenye kuendelea, Wafilisti wametafuta kwa nia ya mubaya* kuleta kisasi na uharibifu.+ 16 Kwa hiyo, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Angalia, ninanyoosha mukono wangu juu ya Wafilisti,+ na nitaondoa Wakereti+ wasikuwe tena na nitaharibu wakaaji wenye kubakia wa eneo la pembeni ya bahari.+ 17 Na nitafanya matendo makubwa ya kisasi juu yao pamoja na azabu kali, nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova wakati nitaleta kisasi changu juu yao.”’”