Ezekieli
35 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, elekeza uso wako kwenye eneo lenye milima la Seiri,+ na utoe unabii juu yake.+ 3 Uliambie, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Angalia, nitapigana na wewe, Ee eneo lenye milima la Seiri, na nitanyoosha mukono wangu juu yako na kukufanya kuwa eneo lenye kuwa ukiwa.+ 4 Nitafanya miji yako kuwa mabomoko, na utakuwa eneo lenye kuwa ukiwa;+ na utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova. 5 Kwa maana ulikuwa na chuki yenye kuendelea,+ na ulitoa Waisraeli ili wauawe kwa upanga wakati wa musiba wao, wakati wa azabu yao ya mwisho.”’+
6 “‘Kwa hiyo kama vile hakika ninaishi,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema, ‘nitakutayarisha kwa ajili ya umwangaji wa damu, na umwangaji wa damu utakufuatilia.+ Kwa maana ulichukia damu, umwangaji wa damu utakufuatilia.+ 7 Nitafanya eneo lenye milima la Seiri kuwa eneo lenye kuwa ukiwa,+ na nitamuondoa katikati yake mutu yeyote mwenye kupita ndani yake na mutu yeyote mwenye kurudia. 8 Nitajaza milima yake watu wenye kuuawa; na wale wenye kuuawa kwa upanga wataanguka kwenye vilima vyako, katika mabonde yako, na katika mito yako yote midogo. 9 Nitakufanya kuwa ukiwa sikuzote, na miji yako haitaikaliwa na watu;+ na mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’
10 “Kwa sababu ulisema, ‘Haya mataifa mbili na inchi hizi mbili zitakuwa zangu, na sisi tutakamata zote mbili,’+ hata kama Yehova mwenyewe alikuwa pale, 11 ‘kwa hiyo kama vile hakika ninaishi,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema, ‘nitakutendea kulingana na kasirani ileile na wivu uleule wenye ulionyesha katika chuki yako kuwaelekea;+ na nitajijulisha kati yao wakati nitakuhukumu. 12 Kisha utalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimesikia mambo yote ya mubaya yenye ulisema kuhusu milima ya Israeli wakati ulisema, “Imeachwa ukiwa na imepewa kwetu ili tuimeze.”* 13 Na mulizungumuza kwa kiburi juu yangu, na muliongeza maneno yenu juu yangu.+ Nilisikia yote.’
14 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Dunia yote itafurahi wakati nitakufanya kuwa eneo lenye kuwa ukiwa. 15 Kama vile ulifurahi wakati uriti wa nyumba ya Israeli uliachwa ukiwa, ni vile nitakutendea.+ Utakuwa mabomoko yenye ukiwa, Ee eneo lenye milima la Seiri, ndiyo, Edomu yote;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”