Ezekieli
44 Akanirudisha kupitia mulango mukubwa wa inje ya patakatifu wenye ulielekea mashariki,+ na ulikuwa umefungwa.+ 2 Kisha Yehova akaniambia: “Mulango huu mukubwa utabakia wenye kufungwa. Hautafunguliwa, na hakuna mwanadamu mwenye ataingia kupitia huo; kwa maana Yehova, Mungu wa Israeli, ameingia kupitia huo,+ kwa hiyo unapaswa kubakia wenye kufungwa. 3 Lakini, mukubwa atakaa katika mulango huo mukubwa ili akule mukate mbele ya Yehova,+ kwa maana yeye ni mukubwa. Ataingia kupitia baraza la mulango mukubwa, na atatoka kupitia baraza hilo.”+
4 Kisha akanileta kupitia mulango mukubwa wa kaskazini mupaka mbele ya hekalu. Wakati niliangalia, nikaona kwamba utukufu wa Yehova ulikuwa umejaza hekalu la Yehova.+ Kwa hiyo nikaanguka uso chini.+ 5 Basi Yehova akaniambia: “Mwana wa binadamu, kaza uangalifu,* angalia, na usikilize muzuri kila kitu chenye nitakuambia kuhusu maagizo na sheria za hekalu la Yehova. Kaza sana uangalifu juu ya njia ya kuingilia ya hekalu na njia zote za kutokea za patakatifu.+ 6 Utaambia nyumba ya Israeli yenye kuasi, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Mazoea yako yenye kuchukiza yametosha, Ee nyumba ya Israeli. 7 Wakati munaleta mahali pangu patakatifu wageni wenye hawatahiriwe katika moyo na katika mwili, wanachafua hekalu langu. Munatoa mukate wangu, mafuta na damu, wakati agano langu linaendelea kuvunjwa kwa sababu ya mazoea yenu yote yenye kuchukiza. 8 Hamujatunza vitu vyangu vitakatifu.+ Kuliko kufanya vile, munapatia wengine migao ya kufanya kazi za patakatifu pangu.”’
9 “‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Mugeni yeyote mwenye kuishi katika Israeli mwenye hatahiriwe katika moyo na katika mwili hataingia patakatifu pangu.”’
10 “‘Lakini Walawi wenye walienda mbali na mimi,+ wakati Israeli walienda mbali na mimi ili kufuata sanamu zao zenye kuchukiza* watapata matokeo ya kosa lao. 11 Nao watakuwa watumishi katika patakatifu pangu ili kusimamia milango mikubwa ya hekalu+ na kufanya utumishi kwenye hekalu. Watachinja toleo nzima la kuteketezwa na zabihu kwa ajili ya watu, nao watasimama mbele ya watu ili kuwatolea utumishi. 12 Kwa sababu waliwatolea utumishi mbele ya sanamu zao zenye kuchukiza na wakakuwa kikwazo chenye kilifanya nyumba ya Israeli itende zambi,+ ndiyo sababu nimeinua mukono wangu juu yao ili kuapa,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema, ‘nao watapata matokeo ya kosa lao. 13 Hawatanikaribia ili kutumika wakiwa makuhani wangu wala kukaribia kitu chochote kati ya vitu vyangu vitakatifu ao vitu vitakatifu zaidi, nao watapata haya yao kwa sababu ya mambo yenye kuchukiza yenye walifanya. 14 Lakini nitawafanya kuwa watu wenye kuwa na daraka la kufanya kazi za hekalu, ili kushugulikia utumishi wake na mambo yote yenye yanapaswa kufanywa ndani.’+
15 “‘Kuhusu makuhani Walawi, wana wa Sadoki,+ wenye walifanya kazi za patakatifu pangu wakati Waisraeli walienda mbali na mimi,+ watanikaribia ili kunitolea utumishi, na watasimama mbele yangu ili kunitolea mafuta+ na damu,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema. 16 ‘Hao ndio wataingia patakatifu pangu, nao watakaribia meza yangu ili kunitolea utumishi,+ na watafanya kazi zenye nimewaomba.+
17 “‘Wakati wanaingia katika milango mikubwa ya kiwanja cha ndani, wanapaswa kuvaa nguo za kitani.+ Hawapaswe kuvaa manyoya yoyote ya kondoo wakati wanafanya utumishi katika milango mikubwa ya kiwanja cha ndani ao ndani ya kiwanja hicho. 18 Wanapaswa kuvaa vilemba vya kitani kwenye kichwa chao, na kapitula za kitani zinapaswa kufunika viuno vyao.+ Hawapaswe kuvaa kitu chochote chenye kufanya jasho iwatoke. 19 Mbele ya kuenda inje kwenye kiwanja cha inje—kiwanja cha inje kwenye watu wanapatikana—wanapaswa kuvua nguo zenye walikuwa wanavaa wakati walikuwa wanafanya utumishi+ na kuzitia katika vyumba vitakatifu vya kukulia chakula.*+ Kisha watavaa nguo zingine, ili wasifanye watu kuwa watakatifu* kupitia nguo zao. 20 Hawapaswe kunyoa kichwa chao+ wala kuacha nywele za kichwa chao zikuwe za murefu. Wanapaswa kupunguza nywele za vichwa vyao. 21 Makuhani hawapaswe kunywa divai wakati wanaingia katika kiwanja cha ndani.+ 22 Hawapaswe kuoa mujane ao mwanamuke mwenye ndoa yake imevunjika;+ lakini wanaweza kuoa bikira wa uzao wa Israeli ao mujane wa kuhani.’+
23 “‘Watafundisha watu wangu kuhusu tofauti kati ya kitu kitakatifu na kitu cha kawaida; na watawafundisha tofauti kati ya kitu chenye hakiko safi na kitu chenye kuwa safi.+ 24 Wanapaswa kusimamia wakiwa waamuzi katika kesi ya hukumu;+ wanapaswa kuhukumu kulingana na maamuzi yangu ya hukumu.+ Wanapaswa kufuata sheria zangu na maagizo yangu kuhusu sikukuu zangu zote+ na kutakasa sabato zangu. 25 Hawapaswe kumukaribia mutu mwenye amekufa, ili wasijichafue. Lakini, wanaweza kujichafua kwa ajili ya baba yao, mama yao, mutoto wao mwanaume, mutoto wao mwanamuke, ndugu yao ao dada yao mwenye hajaolewa.+ 26 Na kisha kutakaswa kwa kuhani, wanapaswa kumuhesabia siku saba (7). 27 Siku yenye anaingia katika mahali patakatifu, katika kiwanja cha ndani, ili kufanya utumishi mahali patakatifu anapaswa kutoa toleo lake la zambi,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.
28 “‘Na huu ndio utakuwa uriti wao: Mimi ndiye uriti wao.+ Musiwapatie mali yoyote katika Israeli, kwa maana mimi ndiye mali yao. 29 Wao ndio watakula toleo la nafaka,+ toleo la zambi, na toleo la hatia,+ na kila kitu chenye kilitolewa katika Israeli kitakuwa chao.+ 30 Matunda ya muzuri sana kati ya matunda yote ya kwanza yenye kukomaa na kila namna ya muchango wenu utakuwa wa makuhani.+ Na mutamupatia kuhani matunda ya kwanza ya unga wenu wa chenga-chenga.+ Hilo litafanya baraka ikuwe juu ya nyumba zenu.+ 31 Makuhani hawapaswe kula ndege ao munyama mwenye alipatikana amekufa ao amepasuliwa vipande-vipande.’+