Ezekieli
6 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, geuzia uso wako kuelekea milima ya Israeli na utoe unabii juu yake. 3 Unapaswa kusema, ‘Enyi milima ya Israeli, musikie neno la Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova: Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anaambia hivi milima, vilima, mito midogo na mabonde: “Angalia! Nitaleta upanga juu yenu, na nitaharibu mahali penu pa juu. 4 Mazabahu zenu zitabomolewa, vinara vyenu vya uvumba vitavunjwa,+ na wenye watauawa kati yenu nitawatupa chini mbele ya sanamu zenu zenye kuchukiza.*+ 5 Nitatupa mizoga ya watu wa Israeli mbele ya sanamu zao zenye kuchukiza, na nitasambaza mifupa yenu kuzunguka pande zote za mazabahu zenu.+ 6 Katika makao yenu yote, miji itaharibiwa+ na mahali pa juu patabomolewa na patabakia pameharibiwa.+ Mazabahu zenu zitabomolewa na kuvunjwa-vunjwa, sanamu zenu zenye kuchukiza zitaangamia, vinara vyenu vya uvumba vitakatwa, na kazi zenu zitafutwa. 7 Na wenye watauawa wataanguka katikati yenu,+ na mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+
8 “‘“Lakini nitaacha mabaki, kwa maana wamoja kati yenu wataponyoka upanga katikati ya mataifa wakati mutasambazwa katika inchi mbalimbali.+ 9 Na wale wenye wataponyoka watanikumbuka kati ya mataifa kwenye wamepelekwa mateka.+ Watatambua kwamba nilikuwa nimevunjika moyo kwa sababu ya moyo wao wa kukosa uaminifu* wenye uliniacha+ na macho yao yenye kutamani sana* sanamu zao zenye kuchukiza.+ Watapata haya na kuchukizwa na mambo yote maovu na yenye kuchukiza yenye wamefanya.+ 10 Watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova na kwamba sikuwaogopesha kwa bure kwamba nitaleta musiba huu juu yao.”’+
11 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Piga mikono na upige vishindo kwa muguu wako na uomboleze kwa sababu ya mambo yote maovu na yenye kuchukiza yenye yalifanywa na nyumba ya Israeli, kwa maana wataanguka kwa upanga, kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza.+ 12 Ule mwenye kuwa mbali atakufa kwa ugonjwa wa kuambukiza, ule mwenye kuwa karibu ataanguka kwa upanga, na mutu yeyote mwenye anaponyoka mambo hayo na kubakia atakufa kwa njaa; na nitamwanga kikamili kasirani yangu kali juu yao.+ 13 Na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,+ wakati wenye watauawa kati yao watalala kati ya sanamu zao zenye kuchukiza, kuzunguka pande zote za mazabahu zao,+ juu ya kila kilima kirefu, juu ya vichwa vyote vya milima, na chini ya kila muti wenye majani mengi, na chini ya matawi ya miti mikubwa kwenye wametoa matoleo yenye harufu ya muzuri* ili kutuliza sanamu zao zote zenye kuchukiza.+ 14 Nitanyoosha mukono wangu juu yao na kufanya inchi ikuwe ukiwa, na makao yao yote yatakuwa mahali kwenye kumekuwa ukiwa kuliko jangwa lenye kuwa karibu na Dibla. Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”