Ezekieli
8 Na katika mwaka wa sita (6), mwezi wa sita, siku ya tano (5) ya mwezi huo, wakati nilikuwa nimekaa katika nyumba yangu na wazee wa Yuda walikuwa wamekaa mbele yangu, mukono wa Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova ulinishika pale. 2 Wakati nilikuwa ninaangalia, niliona umbo yenye ilionekana kama moto; kulikuwa moto chini ya kile chenye kilionekana kuwa kiuno chake,+ na kuanzia kiuno chake kuelekea juu, muonekano wake ulingaa, kama kungaa kwa elektramu.*+ 3 Kisha akanyoosha kile chenye kilionekana kama mukono na kunikamata kwa kishungi cha nywele za kichwa changu, na roho ikanibeba katikati ya dunia na mbingu na kunileta Yerusalemu kupitia maono kutoka kwa Mungu, kwenye muingilio wa mulango mukubwa wa ndani+ wenye unaelekea kaskazini, kwenye alama* ya ibada ya sanamu ya wivu yenye inachochea wivu ilisimama.+ 4 Na angalia! utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa pale,+ kama kuonekana kwenye nilikuwa nimeona katika bonde tambarare.+
5 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, tafazali inua macho yako kuelekea kaskazini.” Basi nikainua macho yangu kuelekea kaskazini, na kule, kaskazini mwa mulango mukubwa wa mazabahu kulikuwa alama* hii ya wivu kwenye muingilio. 6 Naye akaniambia: “Mwana wa binadamu, je, unaona mambo ya mubaya, yenye kuchukiza yenye nyumba ya Israeli inafanya hapa,+ mambo yenye kunifanya niende mbali na patakatifu pangu?+ Lakini utaona mambo ya kuchukiza ya mubaya hata zaidi.”
7 Kisha akanileta kwenye muingilio wa kiwanja, na wakati niliangalia, nikaona tundu katika ukuta. 8 Akaniambia: “Mwana wa binadamu, tafazali toboa ukuta.” Basi nikatoboa ukuta na kuona muingilio. 9 Akaniambia: “Ingia na uone mambo maovu, yenye kuchukiza yenye wanafanya hapa.” 10 Basi nikaingia na kuangalia, na nikaona kila namna ya mifano ya viumbe vyenye kutambaa na wanyama wenye kuchukiza+ na sanamu zote zenye kuchukiza* za nyumba ya Israeli;+ zilikuwa zimechongwa kwenye ukuta kuzunguka pande zote. 11 Na wazee makumi saba (70) wa nyumba ya Israeli walikuwa wamesimama mbele yake, Yaazania mutoto mwanaume wa Shafani+ akiwa amesimama kati yao. Kila mumoja alikuwa na chetezo chake katika mukono wake, na wingu la uvumba lenye marashi lilikuwa linapanda.+ 12 Akaniambia: “Mwana wa binadamu je, unaona mambo yenye wazee wa nyumba ya Israeli wanafanya katika giza, kila mumoja katika vyumba vya ndani kwenye sanamu zake zinaonyeshwa?* Kwa maana wanasema, ‘Yehova hatuone. Yehova ameacha inchi hii.’”+
13 Naye akaendelea kuniambia: “Utaona mambo ya kuchukiza ya mubaya hata zaidi yenye wanafanya.” 14 Kwa hiyo akanileta kwenye muingilio wa mulango mukubwa wa kaskazini wa nyumba ya Yehova, na kule nikaona wanamuke wamekaa wakimulia mungu Tamuzi.
15 Naye akaniambia tena: “Je, unaona jambo hili, Ee mwana wa binadamu? Utaona mambo ya kuchukiza ya mubaya hata zaidi kuliko haya.”+ 16 Basi akanileta katika kiwanja cha ndani cha nyumba ya Yehova.+ Pale kwenye muingilio wa hekalu la Yehova, katikati ya baraza na mazabahu, kulikuwa wanaume karibu makumi mbili na tano (25) wenye migongo yao ilielekea hekalu la Yehova na nyuso zao zilielekea mashariki; nao walikuwa wanainamia jua kuelekea mashariki.+
17 Akaniambia: “Mwana wa binadamu je, unaona jambo hili? Je, ni jambo la kidogo kwa nyumba ya Yuda kufanya mambo haya yenye kuchukiza, kujaza inchi jeuri+ na kuendelea kunikasirisha? Wananyoosha lile tawi* kuelekea pua yangu. 18 Basi nitatenda katika kasirani kali. Jicho langu halitasikitika; wala sitasikia huruma.+ Hata kama wanalia kwa sauti kubwa katika masikio yangu, sitawasikia.”+