Hosea
1 Neno la Yehova lenye lilikuja kwa Hosea* mwana wa Beeri katika siku za Uzia,+ Yotamu,+ Ahazi,+ na Hezekia,+ wafalme wa Yuda,+ na katika siku za Yeroboamu+ mwana wa Yoashi,+ mufalme wa Israeli. 2 Wakati Yehova alianza kusema neno lake kupitia Hosea, Yehova alimuambia Hosea: “Uende, umuoe mwanamuke wa ukahaba* na upate watoto wa ukahaba,* kwa sababu kupitia ukahaba* inchi imegeuka kabisa na kuacha kumufuata Yehova.”+
3 Basi akaenda na kumuoa Gomeri binti ya Diblaimu, na akapata mimba na akamuzalia mutoto mwanaume.
4 Kisha Yehova akamuambia: “Umupatie jina Yezreeli,* kwa maana kisha wakati kidogo nitaomba nyumba ya Yehu itoe hesabu+ kwa sababu ya matendo ya Yezreeli ya umwangaji wa damu, na nitamaliza utawala wa kifalme wa nyumba ya Israeli.+ 5 Siku hiyo nitavunja upinde wa Israeli katika Bonde* la Yezreeli.”
6 Akapata mimba tena na akazaa mutoto mwanamuke. Na Yeye akamuambia: “Umupatie jina Lo-ruhama,* kwa maana sitaonyesha tena nyumba ya Israeli rehema,+ kwa sababu hakika nitawafukuza.+ 7 Lakini nitaonyesha nyumba ya Yuda rehema,+ na nitawaokoa kupitia Yehova Mungu wao;+ sitawaokoa kwa upinde wala kwa upanga wala kwa vita wala kwa farasi wala kwa wapanda-farasi.”+
8 Kisha kumuachisha Lo-ruhama kunyonya, akapata mimba na akazaa mutoto mwanaume. 9 Kisha Yeye akasema: “Umupatie jina Lo-ami,* kwa sababu ninyi hamuko watu wangu na mimi sitakuwa wenu.
10 “Na hesabu ya watu* wa Israeli itakuwa kama chembe za muchanga wa bahari, wenye hauwezi kupimwa wala kuhesabiwa.+ Na mahali kwenye waliambiwa, ‘Ninyi hamuko watu wangu,’+ wataambiwa, ‘Wana wa Mungu mwenye kuishi.’+ 11 Na watu wa Yuda na wa Israeli watakusanywa pamoja katika umoja+ na watajichagulia kichwa kimoja na kupanda kutoka katika inchi, kwa maana siku ya Yezreeli+ itakuwa kubwa.