Hosea
10 “Israeli ni muzabibu wenye kuharibika* wenye unazaa matunda yake.+
Kadiri matunda yake yanaongezeka, ni vile anaongeza mazabahu zake;+
Kadiri inchi yake inazaa muzuri, ni vile nguzo zake takatifu zinakuwa muzuri zaidi.+
Kuko ule mwenye atavunja mazabahu zao na kuharibu nguzo zao.
3 Sasa watasema, ‘Hatuna mufalme,+ kwa maana hatukumuogopa Yehova.
Na mufalme angetufanyia nini?’
4 Wanasema maneno yenye hayana maana, wanaapa viapo vya uongo,+ na wanafanya maagano;
Basi hukumu yenye imechipuka ni kama magugu yenye sumu katika mifereji ya shamba.+
5 Wakaaji wa Samaria wataogopa kwa sababu ya sanamu ya kitoto-dume cha ngombe cha Bet-aveni.+
Watu wake wataiombolezea,
Na vilevile makuhani wake wa mungu wa kigeni wenye walifurahi juu yake na juu ya utukufu wake,
Kwa maana itatoka kwao na kuenda katika uhamisho.
6 Itapelekwa Ashuru kama zawadi kwa mufalme mukubwa.+
Efraimu atapatishwa haya,
Na Israeli atasikia haya kwa sababu ya shauri lenye alifuata.+
7 Samaria na mufalme wake hakika wataharibiwa,*+
Kama tawi lenye lilikatwa lenye kuwa juu ya uso wa maji.
8 Mahali pa juu pa Bet-aveni,+ zambi ya Israeli,+ pataharibiwa.+
Miiba na michongoma itakomaa juu ya mazabahu zao.+
Watu wataambia milima, ‘Mutufunike!’
Na vilima, ‘Mutuangukie!’+
9 Tangu siku za Gibea umetenda zambi,+ Ee Israeli.
Kule waliendelea katika mwenendo uleule.
Vita haikufikia* wana wa ukosefu wa haki katika Gibea.
10 Nitawatia pia nizamu wakati nitapenda.
Na vikundi vya watu vitakusanyika ili kuwashambulia,
Wakati makosa yao mbili yatafungwa kwao.*
11 Efraimu alikuwa kitoto-dike cha ngombe chenye kilizoezwa na chenye kilipenda kukanyanga-kanyanga nafaka,
Basi nililinda shingo yake ya muzuri.
Sasa nitafanya mutu fulani apande* juu ya Efraimu.+
Yuda atalima; Yakobo atamulimia.
12 Mupande mbegu kwa ajili yenu katika haki na muvune upendo mushikamanifu.
Mulime kwa ajili yenu udongo wenye unafaa kulimwa+
Kukiwa bado wakati wa kumutafuta Yehova,+
Mupaka wakati atakuja na kukufundisha haki.+
13 Lakini mumelima uovu,
Mumevuna ukosefu wa haki,+
Na mumekula matunda ya udanganyifu;
Kwa maana mumeweka tegemeo katika njia yenu wenyewe,
Katika wingi wa wapiganaji-vita wenu.
14 Fujo itatokea juu ya watu wako,
Na miji yako yote yenye ngome itaharibiwa,+
Kama vile Shalmani aliharibu nyumba ya Arbeli,
Katika siku ya pigano, wakati mama walivunjwa vipande-vipande pembeni ya watoto wao.
15 Ni vile mutatendewa, Ee Beteli,+ kwa sababu ya uovu wenu mwingi.
Wakati wa mapambazuko* kwa hakika mufalme wa Israeli ataharibiwa.”*+