Hosea
Alitupiga, lakini atafunga vidonda vyetu.
2 Ataturudisha kwenye uzima kisha siku mbili.
Katika siku ya tatu (3) atatuinua,
Na tutaishi mbele yake.
3 Tutajua, tutatafuta kwa bidii kumujua Yehova.
Kutokea kwake ni hakika kama mapambazuko;*
Atakuja kwetu kama mvua kubwa,
Kama mvua ya kipindi cha mvua ya mwisho, yenye inalowanisha dunia.”
4 “Nikufanye nini, Ee Efraimu?
Nikufanye nini, Ee Yuda?
Kwa maana upendo wenu mushikamanifu ni kama mawingu ya asubui,
Kama umande wenye unapotea haraka.
Na hukumu juu yako zitangaa kama mwangaza.+
6 Kwa maana ninapendezwa na upendo mushikamanifu,* hapana zabihu,
Na ujuzi wa Mungu kuliko matoleo mazima ya kuteketezwa.+
7 Lakini wao, kama wanadamu tu, wamevunja agano.+
Pale wamenisaliti.
9 Ushirika wa makuhani ni kama vikundi vya wanyanganyi wenye wanamuvizia mutu.
Wanafanya mauaji katika njia kule Shekemu,+
Kwa maana mwenendo wao ni wa haya.
10 Nimeona jambo la kuchukiza sana katika nyumba ya Israeli.
11 Zaidi ya hayo, Ee Yuda, mavuno yamewekwa kwa ajili yako,
Wakati nitakusanya na kurudisha watu wangu wenye walikamatwa mateka.”+