Yoeli
2 “Mupige baragumu katika Sayuni!+
Mufanye makelele ya vita katika mulima wangu mutakatifu.
Kuko watu wengi na wenye nguvu;+
Hakujakuwa watu kama hao,
Na hakutakuwa tena wengine kama hao
Katika miaka ya vizazi vyote.
3 Mbele yao moto unateketeza,
Na nyuma yao mwali wa moto unateketeza.+
Inchi yenye kuwa mbele yao ni kama bustani ya Edeni,+
Lakini nyuma yao ni kama jangwa lenye kuwa ukiwa,
Hakuna chochote kinaweza kuponyoka.
4 Sura yake ni kama sura ya farasi,
Na wanakimbia kama farasi wa vita.+
5 Sauti yao ni kama ya magari yenye kuruka juu ya milima,+
Kama sauti ya moto wenye kuteketeza majani yenye kukauka.
Ni kama watu wenye nguvu wenye wamejipanga kwa ajili ya vita.+
6 Kwa sababu yao, vikundi vya watu vitakuwa katika uchungu.
Kila uso utakuwa na wasiwasi.
7 Wanakimbia kama wapiganaji-vita,
Wanapanda ukuta kama wanajeshi,
Kila mumoja anabakia katika njia yake,
Na hawabadilishe njia zao.
8 Hawasukumane;
Kila mwanaume anaendelea mbele katika njia yake.
Kama silaha zinafanya wamoja waanguke,
Wengine hawarudie nyuma.
9 Wanaingia haraka katika muji, wanakimbia kwenye ukuta.
Wanapanda juu ya nyumba, na wanaingia kupitia madirisha kama mwizi.
10 Mbele yao inchi inatetemeka na mbingu inatikisika.
Jua na mwezi vimekuwa giza,+
Na nyota zimepoteza mwangaza wake.
11 Yehova atapandisha sauti yake mbele ya jeshi lake,+ kwa maana jeshi lake ni kubwa sana.+
Kwa maana mwenye kutimiza neno Lake ni mwenye nguvu;
Kwa sababu siku ya Yehova ni kubwa na yenye kuogopesha sana.+
Ni nani anaweza kuivumilia?”+
12 “Hata sasa,” ni vile Yehova anasema, “murudie kwangu kwa mioyo yenu yote,+
Kwa kufunga+ na kulia na kuomboleza.
13 Mupasue mioyo yenu,+ hapana nguo zenu,+
Na mumurudilie Yehova Mungu wenu,
Kwa maana yeye ni mwenye huruma* na rehema, hakasirike haraka+ na ni mwenye upendo mwingi mushikamanifu,+
Na atabadilisha nia yake* na hataleta musiba.
14 Ni nani anajua kama hatageuka na kubadilisha nia*+
Na kuwaachia baraka,
Toleo la nafaka na toleo la kinywaji kwa ajili ya Yehova Mungu wenu?
15 Mupige baragumu katika Sayuni!
Mutangaze* kufunga; muite watu kwenye mukusanyiko mukubwa.+
16 Mukusanye watu; mutakase kutaniko.+
Mukusanye wanaume wazee;* mukusanye watoto, na pia watoto wenye kunyonya.+
Bwana-arusi atoke katika chumba chake cha ndani, na bibi-arusi katika chumba chake cha ndoa.
17 Katikati ya baraza na mazabahu,+
Makuhani, watumishi wa Yehova, walie na kusema:
‘Ee Yehova, sikilia watu wako huruma;
Usifanye uriti wako kuwa kitu cha kuzarauliwa,
Kwa kuacha mataifa yawatawale.
Sababu gani vikundi vya watu viseme: “Mungu wao iko* wapi?”’+
18 Kisha Yehova atakuwa na bidii kwa ajili ya inchi yake
Na atasikilia watu wake huruma.+
19 Yehova atajibu watu wake:
‘Angalia, ninawatumia nafaka na divai mupya na mafuta,
Na mutashiba kabisa;+
Sitawafanya tena kuwa kitu cha haya kati ya mataifa.+
20 Nitafukuza mukaaji wa kaskazini mbali na ninyi;
Nitamufukuza mupaka katika eneo lenye kukauka na lenye kuwa ukiwa,
Kikundi chake cha mbele cha walinzi* kuelekea bahari ya mashariki*
Na kikundi chake cha nyuma cha walinzi kuelekea bahari ya mangaribi.*
Harufu ya mubaya sana kutoka kwake itapanda,
Harufu ya mubaya sana kutoka kwake itaendelea kupanda;+
Kwa maana Mungu atafanya mambo makubwa.’
21 Usiogope, Ee inchi.
Shangilia na kufurahi, kwa maana Yehova atafanya mambo makubwa.
22 Musiogope, ninyi wanyama wa pori,
Kwa maana malisho ya jangwa yatakuwa na majani ya mubichi,+
Na miti itazaa matunda;+
Miti ya tini na mizabibu itazaa matunda mengi.+
23 Ninyi wana wa Sayuni, mukuwe na shangwe na mushangilie katika Yehova Mungu wenu;+
Kwa maana atawapatia mvua ya kutosha ya kipindi cha mvua ya kwanza,
Na ataleta mvua kubwa,
Mvua ya kipindi cha mvua ya kwanza na mvua ya kipindi cha mvua ya mwisho, kama zamani.+
24 Viwanja vya kupigia-pigia nafaka vitajaa nafaka safi,
Na vikamulio vitajaa sana divai mupya na mafuta.+
25 Na nitawalipa kwa ajili ya miaka
Yenye nzige mwenye kupatikana kwa wingi, nzige mwenye hana mabawa, na nzige mwenye kula sana, na nzige mwenye kumeza kila kitu amekula,
Jeshi langu kubwa lenye nilituma kati yenu.+
26 Kwa kweli mutakula na kushiba,+
Na mutasifu jina la Yehova Mungu wenu,+
Mwenye amewatendea mambo ya ajabu;
Watu wangu hawatapatishwa haya tena hata siku moja.+
Watu wangu hawatapatishwa haya tena hata siku moja.
28 Kisha nitamwanga roho yangu+ juu ya kila namna ya mwili,
Na watoto wenu wanaume na watoto wenu wanamuke watatoa unabii,
Wazee wenu wataota ndoto,
Na vijana wenu wanaume wataona maono.+
29 Na hata juu ya watumwa wangu wanaume na watumwa wangu wanamuke
Nitamwanga roho yangu katika siku hizo.
30 Na nitatoa maajabu katika mbingu na juu ya dunia,
Damu na moto na nguzo za moshi.+