Mambo ya Walawi
21 Yehova akaendelea kumuambia Musa: “Sema na wana wa Haruni, makuhani, na uwaambie, ‘Mutu yeyote asijichafue kwa ajili ya mutu mwenye alikufa* kati ya watu wake.+ 2 Lakini anaweza kufanya vile kwa ajili ya mutu wa karibu mwenye iko* na uhusiano wa damu pamoja naye, kwa ajili ya mama yake, baba yake, mutoto wake mwanaume, mutoto wake mwanamuke, ndugu yake, 3 na anaweza kujichafua kwa ajili ya dada yake kama ni bikira wa jamaa yake ya karibu na hajaolewa. 4 Hapaswe kujichafua na kujifanya asikuwe safi kwa ajili ya mwanamuke mwenye kuwa na bwana katikati ya watu wake. 5 Hawapaswe kujifanyia upara kwenye vichwa vyao+ ao kunyoa mwisho-mwisho wa ndevu zao ao kujikata-kata mwili.+ 6 Wanapaswa kuwa watakatifu mbele ya Mungu wao,+ na hawapaswe kuchafua jina la Mungu wao,+ kwa sababu wanatoa matoleo ya Yehova yenye yanatolewa kwa njia ya moto, mukate wa* Mungu wao, na wanapaswa kuwa watakatifu.+ 7 Hawapaswe kumuoa kahaba,+ mwanamuke mwenye amechafuliwa, ao mwanamuke mwenye ndoa yake imevunjika,+ kwa sababu kuhani ni mutakatifu mbele ya Mungu wake. 8 Munapaswa kumutakasa kuhani,+ kwa sababu ni yeye anatoa mukate wa Mungu wenu. Munapaswa kumuona kuwa mutakatifu, kwa sababu mimi, Yehova, mwenye anawatakasa ninyi, niko mutakatifu.+
9 “‘Sasa kama binti ya kuhani anajichafua kwa kufanya ukahaba, anamuchafua baba yake. Anapaswa kuteketezwa ndani ya moto.+
10 “‘Kuhani mukubwa mwenye kuwa katikati ya ndugu zake, mwenye mafuta ya kutia mafuta yamemwangwa kwenye kichwa chake+ na mwenye amewekwa katika madaraka* ili avae nguo za ukuhani,+ hapaswe kuacha nywele zake katika hali ya ovyo-ovyo ao kupasua nguo zake.+ 11 Hapaswe kumukaribia mutu yeyote mwenye amekufa;*+ hapaswe hata kujichafua kwa ajili ya baba yake ao mama yake. 12 Hapaswe kutoka patakatifu na hapaswe kuchafua patakatifu pa Mungu wake,+ kwa sababu ile alama ya kuwekwa pembeni kwa ajili ya kusudi la pekee, yale mafuta ya Mungu wake ya kutia mafuta,+ yako juu yake. Mimi ni Yehova.
13 “‘Anapaswa kuoa mwanamuke mwenye kuwa bikira.+ 14 Hapaswe kuoa mwanamuke mujane, mwanamuke mwenye ndoa yake imevunjika, mwenye amechafuliwa, ao kahaba; lakini anapaswa kuchukua bikira katikati ya watu wake ili akuwe bibi yake. 15 Hapaswe kuchafua uzao wake* kati ya watu wake,+ kwa sababu mimi ni Yehova, mwenye kumutakasa.’”
16 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 17 “Ambia Haruni, ‘Mutu yeyote wa uzao wako* katika vizazi vyao vyote mwenye kuwa na kasoro asikaribie ili kutoa mukate wa Mungu wake. 18 Kama kuko mutu fulani mwenye kuwa na kasoro, hapaswe kukaribia: mutu mwenye kuwa kipofu ao kilema wa miguu ao mwenye kuwa na uso wenye kuharibika* ao mwenye kiungo kimoja kirefu sana, 19 mutu mwenye kuvunjika muguu ao mwenye kuvunjika mukono, 20 ao mwenye mugongo wenye kujikunja ao mutu mudogo sana,* ao mutu mwenye kasoro ya macho ao mwenye ukurutu wa ngozi* ao mwenye imba ao mwenye mapumbu yenye kuharibika.+ 21 Mutu yeyote wa uzao wa* Haruni kuhani mwenye kuwa na kasoro hatakaribia ili kutoa matoleo ya Yehova yenye yanatolewa kwa njia ya moto. Kwa sababu iko* na kasoro, hapaswe kukaribia ili kutoa mukate wa Mungu wake. 22 Anaweza kula mukate wa Mungu wake kutoka kati ya vitu vitakatifu sana+ na kutoka kati ya vitu vitakatifu.+ 23 Lakini, hapaswe kukaribia pazia,+ na hapaswe kukaribia mazabahu,+ kwa sababu iko* na kasoro ndani yake; na hapaswe kuchafua patakatifu pangu,+ kwa kuwa mimi ni Yehova, mwenye kuwatakasa.’”+
24 Basi Musa akasema na Haruni na wana wake na Waisraeli wote.