Zekaria
10 “Mumuombe Yehova mvua katika kipindi cha mvua ya mwisho.
Yehova ndiye anafanya mawingu ya zoruba,
Yeye ndiye anawamwangia mvua,+
Na kupatia kila mutu mimea katika shamba.
Wanasema juu ya ndoto za bure,
Na wanajaribu kutoa faraja lakini wanashindwa.
Ndiyo sababu watatanga-tanga kama kondoo.
Watateseka, kwa maana hakuna muchungaji.
3 Kasirani yangu inawaka juu ya wachungaji,
Na nitaomba viongozi wenye kukandamiza* watoe hesabu;
Kwa maana Yehova wa majeshi ameelekeza uangalifu wake kwa kundi lake,+ kwa nyumba ya Yuda,
Na amewafanya kuwa kama farasi wake mwenye heshima katika mapigano.
4 Kutoka kwake kunakuja mutu wa maana,*
Kutoka kwake kunakuja mutawala mwenye kutegemeza,*
Kutoka kwake kunakuja upinde wa vita;
Kwake kunatoka kila mwangalizi,* wote pamoja.
5 Na watakuwa kama wapiganaji-vita,
Wenye wanakanyanga matope ya barabara katika mapigano.
6 Nitafanya nyumba ya Yuda ikuwe yenye nguvu,
Na nitaokoa nyumba ya Yosefu.+
Nitawarudisha,
Kwa maana nitawaonyesha rehema;+
Na watakuwa kama vile sijawakataa hata siku moja;+
Kwa maana mimi ni Yehova Mungu wao, na nitawajibu.
7 Wale wa Efraimu wanapaswa kuwa kama mupiganaji-vita mwenye nguvu,
Na moyo wao utafurahi kama wenye walikunywa divai.+
Wana wao wataona jambo hilo na kufurahi;
Moyo wao utakuwa wenye furaha katika Yehova.+
8 ‘Nitawapigia muluzi na kuwakusanya pamoja;
Kwa maana nitawakomboa,+ na watakuwa wengi,
Na wataendelea kuwa wengi.
9 Hata kama ninawatawanya kama mbegu kati ya vikundi vya watu,
Watanikumbuka wakiwa katika maeneo ya mbali;
Watarudia kwenye uzima pamoja na wana wao na kurudia.
10 Nitawarudisha kutoka inchi ya Misri
Na kuwakusanya kutoka Ashuru;+
Nitawaleta kwenye inchi ya Gileadi+ na Lebanoni,
Na hakutakuwa tena nafasi kwa ajili yao.+
11 Anapaswa kupita katika bahari kwa taabu;
Na ndani ya bahari atapiga mawimbi;+
Sehemu zote za chini kabisa za Muto Nile zitakauka.
Kiburi cha Ashuru kitashushwa,
Na fimbo ya Misri itaondoka.+