Hesabu
18 Kisha Yehova akamuambia Haruni: “Wewe na wana wako na jamaa yako ya upande wa baba mutajibu kwa sababu ya kila kosa lenye litafanywa kuhusu patakatifu,+ na wewe na wana wako mutajibu kwa sababu ya kila kosa lenye litafanywa kuhusu ukuhani wenu.+ 2 Pia uwalete karibu ndugu zako wa kabila la Lawi, kabila la mababu zako, ili wajiunge na wewe+ na kukutumikia wewe na wana wako mbele ya hema ya Ushuhuda.+ 3 Wanapaswa kutimiza madaraka yao kukuelekea na kuelekea hema yote.+ Lakini, hawapaswe kukaribia vyombo vya mahali patakatifu na mazabahu, kusudi ninyi pamoja nao musikufe.+ 4 Watajiunga na wewe na kutimiza madaraka yao kuhusiana na hema ya mukutano na utumishi wote wa hema hiyo, na mutu yeyote mwenye haruhusiwe* hapaswe kuwakaribia ninyi.+ 5 Munapaswa kutimiza daraka lenu kuelekea mahali patakatifu+ na mazabahu,+ kusudi kasirani isikuje tena+ juu ya watu wa Israeli. 6 Mimi mwenyewe nimechukua ndugu zenu, Walawi, kutoka kati ya Waisraeli kuwa zawadi kwa ajili yenu.+ Wametolewa kwa Yehova ili wafanye utumishi wa hema ya mukutano.+ 7 Wewe na wana wako muko na daraka la kufanya kazi za ukuhani zenye zinahusu mazabahu na vitu vyenye kuwa ndani ya pazia,+ na munapaswa kufanya utumishi huo.+ Nimewapatia utumishi wa ukuhani kama zawadi, na mutu yeyote mwenye haruhusiwe* mwenye atakaribia anapaswa kuuawa.”+
8 Yehova akaendelea kumuambia Haruni: “Mimi mwenyewe nilikuweka usimamie michango yenye inafanywa kwa ajili yangu.+ Nimekupatia wewe na wana wako sehemu fulani ya vitu vyote vitakatifu vyenye Waisraeli wanatoa kama muchango ili vikuwe posho lenu la kudumu.+ 9 Hivi vitakuwa vitu vyenu kutoka katikati ya matoleo yote matakatifu sana yenye yanatolewa kwa njia ya moto: kila toleo lenye wanatoa, kutia ndani matoleo yao ya nafaka+ na matoleo yao ya zambi+ na matoleo yao ya hatia+ yenye wananiletea. Ni vitu vitakatifu sana kwa ajili yako na kwa ajili ya wana wako. 10 Utakula vitu hivyo mahali patakatifu zaidi.+ Kila mwanaume anaweza kuvikula. Vitakuwa vitu vitakatifu kwa ajili yako.+ 11 Vitu hivi pia vitakuwa vyako: zawadi zenye wanatoa pamoja+ na matoleo yote ya kutikiswa+ ya Waisraeli. Nimekupatia wewe na watoto wako wanaume na watoto wako wanamuke vitu hivyo ili vikuwe posho lenu la kudumu.+ Kila mutu mwenye kuwa safi katika nyumba yako anaweza kula vitu hivyo.+
12 “Mafuta yote ya muzuri sana na divai yote mupya ya muzuri sana na nafaka, matunda yao ya kwanza,+ yenye wanamupatia Yehova, ninakupatia wewe.+ 13 Matunda yote ya kwanza yenye kukomaa ya inchi yao, yenye watamuletea Yehova, yatakuwa yako.+ Kila mutu mwenye kuwa safi katika nyumba yako anaweza kula matunda hayo.
14 “Kila kitu chenye kimewekwa kwa ajili ya kusudi takatifu* katika Israeli kitakuwa chako.+
15 “Kila muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote vyenye uzima,*+ mwenye watamutolea Yehova, ikuwe mwanadamu ao munyama, atakuwa wako. Lakini, unapaswa kabisa kumukomboa muzaliwa wa kwanza wa wanadamu,+ na muzaliwa wa kwanza wa wanyama wenye hawako safi.+ 16 Utamukomboa muzaliwa wa kwanza kwa bei ya ukombozi wakati iko* na mwezi mumoja na zaidi, kwa samani yenye ilikadiriwa ya shekeli* tano (5) za feza,+ kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu.* Ni gera* makumi mbili (20). 17 Lakini haupaswe kumukomboa ngombe-dume mwenye ni muzaliwa wa kwanza ao mwana-kondoo dume mwenye ni muzaliwa wa kwanza ao mbuzi mwenye ni muzaliwa wa kwanza.+ Hao ni watakatifu. Utanyunyiza* damu yao kwenye mazabahu,+ na mafuta yao utayachoma kusudi yatoe moshi yakiwa toleo lenye linatolewa kwa njia ya moto ili kuwa harufu ya kumupendeza* Yehova.+ 18 Na nyama yao itakuwa yako.+ Itakuwa yako sawa na kifua cha toleo la kutikiswa na muguu wa kuume. 19 Michango yote mitakatifu yenye Waisraeli watamutolea Yehova,+ nimekupatia wewe na watoto wako wanaume na watoto wako wanamuke kuwa posho lenu la kudumu.+ Ni agano la chumvi lenye kudumu* mbele ya Yehova kwa ajili yako na uzao wako pamoja na wewe.”
20 Yehova akaendelea kumuambia Haruni: “Hautakuwa na uriti katika inchi yao, na hautakuwa na sehemu yoyote ya udongo kati yao.+ Mimi ni fungu lako na uriti wako kati ya Waisraeli.+
21 “Sasa ona kwamba nimepatia wana wa Lawi kila sehemu moja ya kumi (1/10)+ katika Israeli kuwa uriti wao kwa sababu ya utumishi wenye wanatimiza, utumishi wa hema ya mukutano. 22 Watu wa Israeli wasikaribie tena hema ya mukutano, ili wasikuwe na hatia ya zambi na kufa. 23 Walawi peke yao ndio watafanya utumishi wa hema ya mukutano, na wao ndio watajibu kwa ajili ya kosa lao.+ Ni sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote kwamba hawapaswe kukamata uriti kati ya Waisraeli.+ 24 Kwa maana nimepatia Walawi sehemu moja ya kumi (1/10) yenye watu wa Israeli wanamutolea Yehova kuwa muchango ili ikuwe uriti wao. Ndiyo sababu nimewaambia, ‘Hawapaswe kukamata uriti kati ya Waisraeli.’”+
25 Kisha Yehova akamuambia Musa: 26 “Unapaswa kuwaambia Walawi, ‘Mutapokea kutoka kwa Waisraeli sehemu moja ya kumi (1/10) yenye nimewapatia ninyi kutoka kwao ili ikuwe uriti wenu,+ na munapaswa kumutolea Yehova muchango wa sehemu moja ya kumi kutoka katika sehemu hiyo ya kumi (1/10).+ 27 Na sehemu hiyo itaonwa kuwa muchango wenu, kama nafaka kutoka kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka+ ao divai yote yenye inatoka katika kikamulio cha divai ao mafuta yote yenye yanatoka katika kikamulio cha mafuta. 28 Kwa njia hiyo mutamutolea pia Yehova muchango kutoka katika sehemu zote za kumi zenye munapokea kutoka kwa Waisraeli, na kutoka katika sehemu hizo munapaswa kumupatia Haruni kuhani muchango kwa ajili ya Yehova. 29 Mutamutolea Yehova kila namna ya muchango kutoka katika zawadi zote za muzuri sana zenye munapokea+ kuwa kitu kitakatifu.’
30 “Na unapaswa kuwaambia, ‘Wakati munatoa vitu vya muzuri sana kutoka katika zawadi hizo kuwa muchango, basi muchango huo wa Walawi utaonwa kama mbegu kutoka katika kiwanja cha kupigia-pigia nafaka na kama divai yenye inatoka katika kikamulio cha divai ao mafuta yenye yanatoka katika kikamulio cha mafuta. 31 Ninyi na watu wa nyumba zenu munaweza kula vitu hivyo mahali popote, kwa sababu ni malipo kwa ajili ya utumishi wenu kwenye hema ya mukutano.+ 32 Hamutakuwa na hatia ya zambi katika jambo hili wakati wote wenye mutanitolea muchango wa vitu vya muzuri sana kutoka katika zawadi hizo, na hamupaswe kuchafua vitu vitakatifu vya Waisraeli, ili musikufe.’”+