Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Matendo 12
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Matendo

      • Yakobo anauawa; Petro anafungwa katika gereza (1-5)

      • Petro anawekwa huru kwa njia ya muujiza (6-19)

      • Malaika anamupiga Herode (20-25)

Matendo 12:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yoh 15:20

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 77-78

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    15/4/2007, uku. 22

Matendo 12:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mt 20:20-23; Lu 11:49
  • +Mt 4:21

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/1/2012, uku. 11

    Kutoa Ushahidi, uku. 78

    “Kila Andiko,”

    uku. 193-194

Matendo 12:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 12:15; 23:15; Law. 23:6

Matendo 12:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kumupeleka inje ili ahukumiwe.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Lu 21:12

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/1/2012, uku. 11

    Kutoa Ushahidi, uku. 77-78

Matendo 12:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Kor. 1:11

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/1/2012, uku. 11

    Kutoa Ushahidi, uku. 79

Matendo 12:6

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 77, 79-80

Matendo 12:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 34:7; Ebr 1:7, 14
  • +Mdo 5:18, 19

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/1/2012, uku. 12

Matendo 12:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Ujifunge.”

Matendo 12:10

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 83

Matendo 12:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Pe. 2:9

Matendo 12:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 13:5; 15:37, 38; Kol 4:10

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/3/2010, uku. 6-7

    1/2/2008, uku. 24

    1/3/2000, uku. 16

    Kutoa Ushahidi, uku. 18, 80, 118

Matendo 12:13

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/3/2010, uku. 7

    Kutoa Ushahidi, uku. 80-81

Matendo 12:14

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 80-81

Matendo 12:15

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 80-81

    Munara wa Mulinzi,

    1/6/2005, uku. 31

Matendo 12:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mt 13:55; Mdo 15:13; 21:18; 1 Kor. 15:7; Gal 1:19; 2:9

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 81, 112

Matendo 12:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 16:27

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 81

Matendo 12:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “alitaka kupigana na.”

  • *

    Tnn., “chumba cha kulala cha mufalme.”

Matendo 12:21

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Amuka!,

    4/2011, uku. 12

    Kutoa Ushahidi, uku. 81-82

Matendo 12:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Amuka!,

    4/2011, uku. 12

    Kutoa Ushahidi, uku. 82

Matendo 12:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza A5.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 6:7; 19:20; Kol 1:6

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 82

Matendo 12:25

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 4:36, 37
  • +Mdo 11:29, 30
  • +Mdo 13:5; 15:37, 38

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/3/2010, uku. 7

    Kutoa Ushahidi, uku. 118

    “Kila Andiko,” uku. 217

Maandiko ingine

Mdo. 12:1Yoh 15:20
Mdo. 12:2Mt 20:20-23; Lu 11:49
Mdo. 12:2Mt 4:21
Mdo. 12:3Kut 12:15; 23:15; Law. 23:6
Mdo. 12:4Lu 21:12
Mdo. 12:52 Kor. 1:11
Mdo. 12:7Zab 34:7; Ebr 1:7, 14
Mdo. 12:7Mdo 5:18, 19
Mdo. 12:112 Pe. 2:9
Mdo. 12:12Mdo 13:5; 15:37, 38; Kol 4:10
Mdo. 12:17Mt 13:55; Mdo 15:13; 21:18; 1 Kor. 15:7; Gal 1:19; 2:9
Mdo. 12:19Mdo 16:27
Mdo. 12:24Mdo 6:7; 19:20; Kol 1:6
Mdo. 12:25Mdo 4:36, 37
Mdo. 12:25Mdo 11:29, 30
Mdo. 12:25Mdo 13:5; 15:37, 38
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Matendo 12:1-25

Matendo ya Mitume

12 Karibu na wakati huo, Mufalme Herode akaanza kutesa wamoja kati ya watu wa kutaniko.+ 2 Aliua kwa upanga+ Yakobo ndugu ya Yohana.+ 3 Wakati aliona kuwa jambo hilo limependeza Wayahudi, akamukamata Petro pia. (Hiyo ilikuwa katika siku za Mikate Yenye Haina Chachu.)+ 4 Akamukamata na kumutia katika gereza.+ Vikundi ine (4) vya maaskari vilikuwa vinamuchunga kwa kubadilishana; kila kikundi kilikuwa na maaskari ine, na alikusudia kumupeleka inje* mbele ya watu kisha Pasaka. 5 Kwa hiyo, Petro alikuwa katika gereza, lakini kutaniko lilikuwa linasali kwa Mungu kwa bidii sana kwa ajili yake.+

6 Wakati Herode alikuwa karibu kumupeleka inje, usiku huo Petro alikuwa amelala akiwa amefungwa kwa minyororo mbili katikati ya maaskari wawili, na walinzi wenye walikuwa mbele ya mulango walikuwa wanalinda gereza. 7 Lakini angalia! malaika wa Yehova* alikuwa amesimama pale,+ na mwangaza ukangaa katika chumba cha gereza. Akamupiga Petro kwenye ubavu, akamuamusha, kwa kusema: “Simama mbio!” Na minyororo ikaanguka kutoka kwenye mikono yake.+ 8 Malaika akamuambia: “Vaa nguo* na uvae viatu vyako.” Akafanya vile. Mwishowe akamuambia: “Vaa nguo yako ya inje, na uendelee kunifuata.” 9 Na akatoka na akaendelea kumufuata, lakini hakujua kwamba mambo yenye malaika alikuwa anafanya yalikuwa ya kweli. Kwa kweli, aliwaza alikuwa anaona maono. 10 Wakapita mulinzi wa kwanza na wa pili, wakafika kwenye mulango mukubwa wa chuma wenye kupeleka kwenye muji, na ukafunguka wenyewe mbele yao. Kisha wao kutoka inje, wakaenda na kupita katika njia moja, na mara moja ule malaika akamuacha. 11 Na Petro, wakati alitambua kile kilikuwa kinafanyika, akasema: “Sasa ninajua kwa hakika kwamba Yehova* alimutuma malaika wake na kunikomboa kutoka katika mukono wa Herode na kutoka katika mambo yote yenye Wayahudi walikuwa wanatazamia yatokee.”+

12 Kisha kutambua jambo hilo, akaenda kwenye nyumba ya Maria mama ya Yohana mwenye aliitwa Marko;+ mule watu fulani walikuwa wamekusanyika pamoja na walikuwa wanasali. 13 Wakati alipiga hodi kwenye mulango wa muingilio wa mulango mukubwa, mutumishi mwanamuke mwenye kuitwa Roda akaenda kuona ni nani. 14 Wakati alitambua sauti ya Petro, akafurahi sana na hivyo hakufungua mulango mukubwa, lakini akakimbia ndani mbio na kuwaelezea kwamba Petro amesimama kwenye muingilio wa mulango mukubwa. 15 Wakamuambia: “Umepoteza akili.” Lakini akaendelea kusema kwa mukazo kwamba ni kweli. Wakaanza kusema: “Ni malaika wake.” 16 Lakini Petro akabakia pale akipiga hodi. Wakati walifungua mulango, wakamuona na wakashangaa. 17 Lakini akawafanyia alama kwa mukono wanyamaze na akawaambia kwa urefu namna Yehova* alimutosha katika gereza, na akasema: “Muambie Yakobo+ na ndugu mambo haya.” Basi akatoka na kusafiri ili kuenda mahali pengine.

18 Sasa wakati ilikuwa muchana, maaskari wakakuwa katika muvurugo kwa sababu hawakujua ni mambo gani yalimupata Petro. 19 Herode akamutafuta kila mahali, na wakati alimukosa, akauliza walinzi maulizo na akaamuru wapelekwe ili wapewe azabu;+ na akashuka kutoka Yudea na kuenda Kaisaria, akakaa kule kwa wakati fulani.

20 Sasa Herode alikuwa amekasirikia* watu wa Tiro na Sidoni. Basi wakakuja kwake wakiwa na kusudi moja, na kisha kumusadikisha Blasto, mwanaume mwenye kusimamia nyumba ya mufalme,* wakatoa ombi la kufanya amani, kwa sababu inchi yao ilikuwa inapata chakula kutoka katika inchi ya mufalme. 21 Siku moja yenye ilichaguliwa, Herode alivaa nguo ya kifalme na kukaa kwenye kiti cha hukumu na kuanza kutolea watu hotuba ya watu wote. 22 Kisha watu wenye walikuwa wamekusanyika wakaanza kusema kwa sauti kubwa: “Hii ni sauti ya mungu, haiko ya mwanadamu!” 23 Mara moja malaika wa Yehova* akamupiga, kwa sababu hakumupatia Mungu utukufu, na vidudu vikamukula na akakufa.

24 Lakini neno la Yehova* likaendelea kuongezeka na kuenea.+

25 Kisha Barnaba+ na Sauli kutimiza kabisa-kabisa kazi ya kutoa misaada kule Yerusalemu,+ wakarudia na kumuchukua Yohana,+ mwenye aliitwa pia Marko, na wakaenda pamoja naye.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine