Waamuzi
17 Kulikuwa mutu mumoja katika eneo lenye milima la Efraimu+ mwenye aliitwa Mika. 2 Akamuambia mama yake: “Vile vipande elfu moja na mia moja (1 100) vya feza vyenye vilikamatwa kutoka kwako na ukasema maneno ya kulaani, yenye nilisikia—angalia! niko na feza hiyo. Ni mimi niliikamata.” Kwa hiyo, mama yake akasema: “Yehova abariki mwana wangu.” 3 Basi akarudishia mama yake vile vipande elfu moja na mia moja (1 100) vya feza, lakini mama yake akasema: “Hakika nitatakasa kwa ajili ya Yehova feza hiyo yenye kutoka katika mukono wangu ili mwana wangu aitumie kutengeneza sanamu ya kuchongwa na sanamu ya metali.*+ Sasa nitarudisha feza hiyo kwako.”
4 Kisha yeye kurudishia mama yake feza hiyo, mama yake akakamata vipande mia mbili (200) vya feza na kuvipatia fundi wa feza. Fundi huyo akatengeneza sanamu ya kuchongwa na sanamu ya metali;* na sanamu hizo zikawekwa katika nyumba ya Mika. 5 Mutu huyo Mika alikuwa na nyumba ya miungu, na alitengeneza efodi+ na sanamu za terafimu*+ na kuweka* mumoja wa wana wake akuwe kuhani wake.+ 6 Katika siku hizo hapakukuwa mufalme katika Israeli.+ Kila mutu alikuwa anafanya jambo lenye lilikuwa sawa mbele ya macho yake mwenyewe.*+
7 Basi kulikuwa kijana fulani mwanaume wa Betlehemu+ katika Yuda, alikuwa wa familia ya Yuda. Alikuwa Mulawi+ mwenye alikuwa ameishi pale kwa muda. 8 Kijana huyo akaondoka katika muji wa Betlehemu katika Yuda ili atafute mahali pa kuishi. Wakati alikuwa katika safari yake, alifika katika eneo lenye milima la Efraimu, kwenye nyumba ya Mika.+ 9 Kisha Mika akamuuliza: “Unatoka wapi?” Akamujibu: “Mimi ni Mulawi kutoka Betlehemu katika Yuda, niko katika safari ili kutafuta mahali pa kuishi.” 10 Basi Mika akamuambia: “Kaa pamoja na mimi, na ukuwe kama baba* na kuhani wangu. Nitakupatia vipande kumi (10) vya feza kwa mwaka na furushi la nguo, na pia chakula chako.” Kwa hiyo Mulawi huyo akaingia ndani. 11 Basi Mulawi huyo akakubali kukaa na mutu huyo, na kijana huyo mwanaume akakuwa kama mumoja wa wana wake. 12 Zaidi ya hayo, Mika akamuweka* Mulawi huyo kuwa kuhani wake,+ na akaishi katika nyumba ya Mika. 13 Basi Mika akasema: “Sasa ninajua kwamba Yehova atanitendea mema, kwa maana Mulawi amekuwa kuhani wangu.”