Cha Kwanza cha Samweli
28 Siku hizo Wafilisti walikusanya majeshi yao ili kupigana vita na Israeli.+ Kwa hiyo Akishi akamuambia Daudi: “Unajua, kwa kweli, kwamba wewe na watu wako mutaenda katika vita pamoja na mimi.”+ 2 Basi Daudi akamuambia Akishi: “Hakika unajua jambo lenye mutumishi wako atafanya.” Akishi akamuambia Daudi: “Ndiyo sababu nitakuweka kuwa mulinzi wangu wa kudumu.”*+
3 Wakati huo Samweli alikuwa amekufa, na Israeli wote walikuwa wamemuombolezea na kumuzika katika Rama, muji wake mwenyewe.+ Na Sauli alikuwa ameondoa katika inchi watu wenye kupashana habari na pepo wachafu na watu wenye kutabiri matukio.+
4 Wafilisti wakakusanyika na wakaenda na kupiga kambi Shunemu.+ Kwa hiyo Sauli akakusanya Israeli wote, nao wakapiga kambi Gilboa.+ 5 Wakati Sauli aliona kambi ya Wafilisti, akaogopa, na moyo wake ukatetemeka sana.+ 6 Ijapokuwa Sauli alikuwa anamuuliza Yehova,+ Yehova hakumujibu hata mara moja, ikuwe katika ndoto ao kwa Urimu+ ao kupitia manabii. 7 Mwishowe Sauli akaambia watumishi wake: “Munitafutie mwanamuke mwenye kupashana habari na pepo wachafu,+ nitaenda na kumuomba shauri.” Watumishi wake wakajibu: “Angalia! Kule En-dori kuko mwanamuke mwenye kupashana habari na pepo wachafu.”+
8 Kwa hiyo Sauli akajifanya wasimutambue na akavaa nguo zingine na kuenda kwa mwanamuke huyo usiku akiwa na watu wake wawili. Akasema: “Fanya uaguzi, tafazali, kwa kupashana habari na pepo wachafu,+ na unipandishie ule mwenye nitakutajia.” 9 Lakini, mwanamuke huyo akamuambia: “Unapaswa kujua mambo yenye Sauli alifanya, namna aliondoa katika inchi watu wenye kupashana habari na pepo wachafu na watu wenye kutabiri matukio.+ Sababu gani, basi, unajaribu kunitega* ili niuawe?”+ 10 Basi Sauli akamuapia katika jina la Yehova, kwa kusema: “Kama vile hakika Yehova anaishi, hautakuwa na hatia yoyote katika jambo hili!” 11 Halafu mwanamuke huyo akasema: “Nikupandishie nani?” Akajibu: “Unipandishie Samweli.” 12 Wakati mwanamuke huyo alimuona “Samweli,”*+ akalalamika kwa sauti yake yote na kumuambia Sauli: “Sababu gani ulinidanganya? Wewe ni Sauli!” 13 Mufalme akamuambia: “Usiogope, lakini unaona nini?” Mwanamuke huyo akamujibu Sauli: “Ninaona mutu fulani kama mungu akipanda kutoka katika dunia.” 14 Mara moja Sauli akamuuliza mwanamuke huyo: “Iko* namna gani?” akamuambia: “Ni mwanaume muzee mwenye kupanda juu, na amevaa koti yenye haina mikono.”+ Basi Sauli akatambua kwamba alikuwa “Samweli,” na akainamisha uso wake mupaka chini na kuinama uso chini.
15 Kisha “Samweli” akamuambia Sauli: “Sababu gani umenisumbua kwa kufanya nipandishwe?” Sauli akajibu: “Niko katika taabu kubwa. Wafilisti wanapigana na mimi, na Mungu ameniacha na hanijibu tena, ikuwe kupitia manabii ao katika ndoto;+ ndiyo sababu nimekuita unijulishe jambo lenye ninapaswa kufanya.”+
16 Na “Samweli” akasema: “Sababu gani unaniuliza wakati wenye Yehova amekuacha+ na amekuwa adui yako? 17 Yehova atajifanyia mwenyewe mambo yenye alitabiri kupitia mimi: Yehova ataondoa ufalme katika mikono yako na kuupatia mwenzako, Daudi.+ 18 Kwa sababu haukutii sauti ya Yehova na haukutimiza kasirani yake yenye kuwaka juu ya Waamaleki,+ ndiyo sababu Yehova anakutendea mambo haya leo. 19 Pia, Yehova atakutia wewe na Israeli katika mukono wa Wafilisti,+ na kesho wewe+ na wana wako+ mutakuwa pamoja na mimi. Yehova atatia pia jeshi la Israeli katika mikono ya Wafilisti.”+
20 Mara moja Sauli akaanguka chini akiwa amenyooka mwili muzima na akaogopa sana kwa sababu ya maneno ya “Samweli.” Na nguvu zikamuishia, kwa sababu hakukuwa amekula chakula muchana wote na usiku wote. 21 Wakati mwanamuke huyo alikuja mbele ya Sauli na kuona kwamba amevurugika sana, akamuambia: “Mimi mutumishi wako nimetii jambo lenye ulisema, na nimetia uzima wangu katika hatari*+ na kufanya jambo lenye uliniambia nifanye. 22 Sasa, tafazali, sikiliza maneno yenye mutumishi wako anataka kusema. Acha nitie mbele yako kipande cha mukate; kisha ukule ili upate nguvu kidogo ya kuendelea na safari yako.” 23 Lakini akakataa na kusema: “Sitakula.” Hata hivyo, watumishi wake na pia mwanamuke huyo wakaendelea kumukaza. Mwishowe akawasikiliza na kusimama kutoka chini na kukaa kwenye kitanda. 24 Mwanamuke huyo alikuwa na kitoto-dume cha ngombe chenye kunenepa katika nyumba yake, basi akakichinja* haraka na kukamata unga na kutengeneza donge na kupika mikate yenye haina chachu. 25 Akamupatia Sauli na watumishi wake, nao wakakula. Kisha wakasimama na kuenda usiku huo.+