24 ‘Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, umeanza kumuonyesha mutumishi wako ukubwa wako na mukono wako wenye nguvu,+ kwa maana ni mungu gani katika mbingu ao juu ya dunia mwenye anatenda matendo yenye nguvu kama wewe?+
22 Ndiyo sababu wewe kwa kweli ni mukubwa,+ Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova. Hakuna mwenye kuwa kama wewe,+ na hakuna Mungu isipokuwa wewe;+ mambo yote yenye tumesikia kwa masikio yetu yanahakikisha jambo hilo.