-
Kutoka 29:16-18Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
16 Uchinje ule kondoo na ukamate damu yake na kuinyunyiza* kwenye pande zote za mazabahu.+ 17 Kata ule kondoo vipande-vipande, na usafishe matumbotumbo yake+ na miguu yake, na upange vipande hivyo pamoja na kichwa chake. 18 Unapaswa kuchoma kondoo yote muzima, ili itoe moshi kwenye mazabahu. Ni toleo la kuteketezwa kwa ajili ya Yehova, harufu ya muzuri.*+ Ni toleo lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto.
-
-
Mambo ya Walawi 8:18-21Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
18 Sasa akaleta kondoo-dume wa toleo la kuteketezwa karibu, na Haruni na wana wake wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo-dume huyo.+ 19 Kisha Musa akamuchinja na kunyunyiza* damu yake kwenye pande zote za mazabahu. 20 Akakata kondoo-dume huyo vipande-vipande, na Musa akachoma kichwa, vile vipande, na yale mafuta* ili yatoe moshi. 21 Akasafisha matumbotumbo na miguu kwa maji, na Musa akachoma kondoo-dume muzima ili atoe moshi juu ya mazabahu. Lilikuwa toleo la kuteketezwa lenye harufu ya muzuri.* Lilikuwa toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.
-
-
Mambo ya Walawi 9:12-14Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
12 Kisha akachinja toleo la kuteketezwa, na wana wa Haruni wakamupatia damu, na akainyunyiza* kwenye pande zote za mazabahu.+ 13 Wakamupatia vipande vya toleo la kuteketezwa pamoja na kichwa, na akavichoma ili vitoe moshi juu ya mazabahu. 14 Pia, akasafisha matumbotumbo na miguu na akachoma vitu hivyo juu ya toleo la kuteketezwa ili vitoe moshi juu ya mazabahu.
-