Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 25:35
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 35 “‘Kama ndugu yako mwenye kuwa karibu anakuwa maskini na hawezi kujitegemeza, unapaswa kumutegemeza,+ kama vile ungemutegemeza mukaaji mugeni na muhamiaji,+ ili aendelee kuwa muzima pamoja na wewe.

  • Mezali 19:17
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 17 Mwenye anaonyesha mutu wa hali ya chini wema anamukopesha Yehova,+

      Na Yeye atamulipa* kwa sababu ya mambo yenye anatenda.+

  • Matayo 5:42
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 42 Upatie mwenye anakuomba, na usimugeuzie mugongo mutu mwenye anataka umukopeshe.*+

  • Luka 6:34, 35
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 34 Pia, kama munakopesha* wale wenye munatumaini watawalipa, hilo linawapatia ninyi sifa gani?+ Hata watenda-zambi wanakopesha watenda-zambi wenzao ili wawarudishie kiasi kilekile. 35 Tofauti na hilo, muendelee kupenda maadui wenu, kutenda mema, na kukopesha bila kutumaini kurudishiwa kitu chochote;+ na zawabu yenu itakuwa kubwa, na mutakuwa wana wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi, kwa maana yeye ni mwenye fazili kuelekea watu wenye hawana shukrani na waovu.+

  • Wagalatia 2:10
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 10 Walituomba tu kwamba tukumbuke maskini, na mimi nimejikaza sana kufanya vile.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine