-
Hesabu 21:33, 34Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
33 Kisha wakageuka na kupanda kupitia Njia ya Bashani. Na Ogu+ mufalme wa Bashani akatoka pamoja na watu wake wote ili kupigana nao kule Edrei.+ 34 Yehova akamuambia Musa: “Usimuogope,+ kwa maana nitamutia yeye na watu wake wote na inchi yake katika mukono wako,+ na utamutendea kama vile ulimutendea Sihoni mufalme wa Waamori, mwenye aliishi Heshboni.”+
-
-
Kumbukumbu la Torati 3:3Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
3 Kwa hiyo Yehova Mungu wetu akamutia pia Mufalme Ogu wa Bashani pamoja na watu wake wote katika mukono wetu, na tukaendelea kumupiga na tukamuua mupaka hapakukuwa mutu katikati ya watu wake mwenye aliokoka.
-
-
Yoshua 9:9, 10Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
9 Basi wakamuambia: “Watumishi wako wametoka katika inchi ya mbali sana+ kwa sababu ya jina la Yehova Mungu wako, kwa sababu tumesikia juu ya sifa zake na mambo yote yenye alitenda kule Misri+ 10 na mambo yote yenye alitendea wale wafalme wawili wa Waamori wenye walikuwa ngambo ingine ya* Yordani, Mufalme Sihoni+ wa Heshboni na Mufalme Ogu+ wa Bashani, mwenye alikuwa Ashtaroti.
-