-
2 Samweli 16:1Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
16 Wakati Daudi alikuwa amepita kidogo kile kichwa cha mulima,+ Siba+ mutumishi wa Mefibosheti,+ alikuwa pale ili kumupokea; alikuwa na punda wawili wenye matandiko, na juu yao kulikuwa mikate mia mbili (200), keki mia moja (100) za zabibu, keki mia moja za matunda ya kipindi cha joto,* na mutungi mukubwa wa divai.+
-
-
2 Samweli 17:27-29Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
27 Wakati tu Daudi alifika Mahanaimu, Shobi mwana wa Nahashi kutoka muji wa Raba+ wa Waamoni, Makiri+ mwana wa Amieli kutoka Lo-debari, na Barzilai+ Mugileadi kutoka Rogelimu 28 wakaleta vitanda, beseni, vyungu vya udongo, ngano, shayiri, unga, nafaka yenye kukaangwa, maharagi ya munene-munene, dengu, nafaka yenye kukauka, 29 asali, siagi, kondoo, na jibini.* Walileta vitu hivyo vyote kwa ajili ya Daudi na watu wenye walikuwa pamoja naye ili wakule,+ kwa maana walisema: “Watu wamesikia njaa na wamechoka na wako na kiu katika jangwa.”+
-