Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 22:18, 19
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 18 Lakini mufalme wa Yuda mwenye aliwatuma ninyi kumuuliza Yehova, ni hivi munapaswa kumuambia, “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Kuhusu maneno yenye umesikia, 19 kwa sababu moyo wako ulikuwa musikivu* na ulijinyenyekeza+ mbele ya Yehova wakati ulisikia mambo yenye nilisema juu ya mahali hapa na wakaaji wake⁠—​kwamba watakuwa kitu cha kuogopesha na laana⁠—​na ukapasua nguo zako+ na kulia mbele yangu, mimi pia nimekusikia, ni vile Yehova anasema.

  • 2 Mambo ya Nyakati 33:13
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 13 Aliendelea kusali kwake Yeye, na Yeye akaguswa na ombi lake na akasikia ombi lake la kuomba rehema, Naye akamurudisha Yerusalemu kwenye ufalme wake.+ Kisha Manase akajua kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli.+

  • Zaburi 22:24
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 24 Kwa maana hajazarau wala kuchukizwa na mateso ya ule mwenye kukandamizwa;+

      Hajamuficha uso wake.+

      Wakati alimulilia amusaidie, alisikia.+

  • Zaburi 34:18
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 18 Yehova iko* karibu na wale wenye kuvunjika moyo;+

      Anaokoa wale wenye kupondwa roho.*+

  • Mezali 28:13
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 13 Mwenye anafunika makosa yake hatafanikiwa,+

      Lakini kila mutu mwenye anayaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.+

  • Isaya 57:15
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 15 Kwa maana ule Mwenye Kuwa Juu na Mwenye Kuinuka Sana,

      Mwenye anaishi* milele+ na mwenye jina lake ni takatifu,+ anasema hivi:

      “Ninaishi mahali kwenye kuinuka na patakatifu,+

      Lakini pia pamoja na wale wenye kupondwa na wenye roho ya unyenyekevu,

      Ili kupatia uzima roho ya watu wa hali ya chini

      Na kupatia uzima moyo wa wale wenye kupondwa.+

  • Luka 15:22-24
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 22 Lakini baba yake akaambia watumwa wake, ‘Haraka! mulete kanzu ya muzuri zaidi na mumuvalishe, na mutie pete kwenye mukono wake na viatu kwenye miguu yake. 23 Mulete pia kitoto-dume cha ngombe chenye kunenepa, mukichinje, tukule na tufurahi, 24 kwa maana huyu mwana wangu alikuwa amekufa lakini amekuwa muzima tena;+ alikuwa amepotea na amepatikana.’ Basi wakaanza kujifurahisha.

  • Luka 18:13, 14
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 13 Hata hivyo ule mukusanya-kodi alikuwa amesimama mbali kidogo, na hakutaka hata kuinua macho yake kuelekea mbinguni, lakini alikuwa anajipiga-piga kwenye kifua, akisema, ‘Ee Mungu, unihurumie, mimi mutenda-zambi.’+ 14 Ninawaambia ninyi, mutu huyu alishuka kuenda kwenye nyumba yake na akaonekana kuwa mwenye haki kuliko ule Mufarisayo.+ Kwa sababu kila mutu mwenye kujiinua atapatishwa haya, lakini kila mutu mwenye kujinyenyekeza atainuliwa.”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine