-
2 Wafalme 22:18, 19Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
18 Lakini mufalme wa Yuda mwenye aliwatuma ninyi kumuuliza Yehova, ni hivi munapaswa kumuambia, “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Kuhusu maneno yenye umesikia, 19 kwa sababu moyo wako ulikuwa musikivu* na ulijinyenyekeza+ mbele ya Yehova wakati ulisikia mambo yenye nilisema juu ya mahali hapa na wakaaji wake—kwamba watakuwa kitu cha kuogopesha na laana—na ukapasua nguo zako+ na kulia mbele yangu, mimi pia nimekusikia, ni vile Yehova anasema.
-
-
Zaburi 22:24Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
Wakati alimulilia amusaidie, alisikia.+
-
-
Luka 15:22-24Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
22 Lakini baba yake akaambia watumwa wake, ‘Haraka! mulete kanzu ya muzuri zaidi na mumuvalishe, na mutie pete kwenye mukono wake na viatu kwenye miguu yake. 23 Mulete pia kitoto-dume cha ngombe chenye kunenepa, mukichinje, tukule na tufurahi, 24 kwa maana huyu mwana wangu alikuwa amekufa lakini amekuwa muzima tena;+ alikuwa amepotea na amepatikana.’ Basi wakaanza kujifurahisha.
-
-
Luka 18:13, 14Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
13 Hata hivyo ule mukusanya-kodi alikuwa amesimama mbali kidogo, na hakutaka hata kuinua macho yake kuelekea mbinguni, lakini alikuwa anajipiga-piga kwenye kifua, akisema, ‘Ee Mungu, unihurumie, mimi mutenda-zambi.’+ 14 Ninawaambia ninyi, mutu huyu alishuka kuenda kwenye nyumba yake na akaonekana kuwa mwenye haki kuliko ule Mufarisayo.+ Kwa sababu kila mutu mwenye kujiinua atapatishwa haya, lakini kila mutu mwenye kujinyenyekeza atainuliwa.”+
-