Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Isaya 2:2, 3
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    •  2 Katika kipindi cha mwisho cha zile siku,

      Mulima wa nyumba ya Yehova

      Utawekwa imara kabisa kwenye kichwa cha milima,+

      Na utainuliwa juu ya vilima,

      Na mataifa yote yatamiminika kule.+

       3 Na vikundi vingi vya watu vitaenda na kusema:

      “Mukuje, tupande kwenye mulima wa Yehova,

      Kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+

      Atatufundisha njia zake,

      Na tutatembea katika mapito yake.”+

      Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,

      Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.+

  • Zekaria 14:9
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 9 Na Yehova atakuwa Mufalme juu ya dunia yote.+ Katika siku hiyo Yehova atakuwa mumoja,+ na jina lake litakuwa moja.+

  • Ufunuo 7:9, 10
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 9 Kisha mambo hayo nikaona, na angalia! kundi kubwa la watu, wenye hakuna mutu mwenye aliweza kuhesabia, kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga,+ wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo, wakiwa wamevaa kanzu za mweupe;+ na kulikuwa matawi ya mitende katika mikono yao.+ 10 Na wanaendelea kusema kwa sauti kubwa: “Wokovu wetu unatoka kwa Mungu wetu, mwenye kukaa kwenye kiti cha ufalme,+ na kwa Mwana-Kondoo.”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine