-
Zaburi 72:1Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
72 Ee Mungu, umupatie mufalme hukumu zako,
Na umupatie mwana wa mufalme haki yako.+
-
-
Mika 4:1-3Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
4 Katika kipindi cha mwisho cha zile siku,*
Mulima wa nyumba ya Yehova+
Utawekwa imara kabisa kwenye kichwa cha milima,
Na utainuliwa juu ya vilima,
Na vikundi vya watu vitamiminika kule.+
2 Na mataifa mengi yataenda na kusema:
“Mukuje, tupande kwenye mulima wa Yehova
Na kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+
Atatufundisha njia zake,
Na tutatembea katika njia zake.”
Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,
Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.
3 Atafanya hukumu kati ya vikundi vingi vya watu+
Na kunyoosha* mambo kuhusu mataifa yenye nguvu yenye kuwa mbali.
Taifa halitainua upanga juu ya taifa,
Wala hawatajifunza vita tena.+
-