-
Yoshua 1:7, 8Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
7 “Ila tu ukuwe hodari na mwenye nguvu sana, na ufuate kwa uangalifu Sheria yote yenye Musa mutumishi wangu alikuamuru. Usiiache kwa kuenda kuume wala kushoto,+ ili utende kwa hekima kila mahali kwenye unaenda.+ 8 Kitabu hiki cha Sheria kisitoke katika kinywa chako,+ na unapaswa kukisoma kwa sauti ya chini* muchana na usiku, ili ufuate kwa uangalifu mambo yote yenye kuandikwa ndani;+ ukifanya vile, njia yako itakuwa na matokeo ya muzuri na utatenda kwa hekima.+
-
-
1 Wafalme 2:3Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
3 Unapaswa kutimiza mambo yenye Yehova Mungu wako anakuomba kwa kutembea katika njia zake na kwa kushika sheria zake, amri zake, hukumu zake, na vikumbusho vyake kama vile vimeandikwa katika Sheria ya Musa;+ halafu utapata matokeo ya muzuri* katika kila jambo lenye unafanya na kila mahali kwenye unageuka kuenda.
-
-
Zaburi 119:100Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
100 Ninatenda kwa uelewaji mwingi kuliko wanaume wazee,
Kwa sababu ninashika maagizo yako.
-