-
1 Samweli 23:26-28Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
26 Wakati Sauli alifika upande mumoja wa mulima, Daudi na watu wake walikuwa upande mwingine wa mulima huo. Daudi alikuwa anafanya haraka ili kumukimbia+ Sauli, lakini Sauli na watu wake walikuwa wanamuzunguka Daudi na watu wake ili wawakamate.+ 27 Lakini mujumbe fulani akakuja kwa Sauli, na kusema: “Kuja haraka, kwa sababu Wafilisti wamekuja kushambulia inchi!” 28 Basi Sauli akaacha kumufuatilia Daudi+ na akaenda kupigana na Wafilisti. Ndiyo sababu mahali pale paliitwa Mwamba wa Migawanyiko.
-
-
2 Samweli 17:21, 22Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
21 Kisha watu hao kuenda, walitoka katika kisima na kuenda na kumujulisha Mufalme Daudi. Wakamuambia: “Musimame na muvuke haraka maji haya, kwa maana hili ndilo shauri lenye Ahitofeli alitoa juu yenu.”+ 22 Mara moja Daudi na watu wote wenye walikuwa pamoja naye wakasimama na kuvuka Yordani. Kufikia asubui sana, hakuna hata mutu mumoja mwenye hakukuwa amevuka Yordani.
-