-
Mwanzo 20:6Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
6 Basi Mungu wa kweli akamuambia katika ndoto: “Ninajua kwamba ulifanya vile kwa moyo muzuri, kwa hiyo nilikuzuia usinitendee zambi. Ndiyo sababu sikukuruhusu umuguse.
-
-
2 Mambo ya Nyakati 26:16-18Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
16 Hata hivyo, wakati tu alikuwa na nguvu, moyo wake ukakuwa na majivuno na kufikia kuleta uharibifu wake mwenyewe, na alitenda kwa kukosa uaminifu kumuelekea Yehova Mungu wake kwa kuingia katika hekalu la Yehova ili kuchoma uvumba kwenye mazabahu ya uvumba.+ 17 Mara moja Azaria kuhani na makuhani wengine makumi munane (80) wa Yehova wenye uhodari wakamufuata ndani. 18 Wakapambana na Mufalme Uzia na kumuambia: “Haiko kazi yako, Uzia, kumuchomea Yehova uvumba!+ Ni makuhani tu ndio wanapaswa kuchoma uvumba, kwa maana wao ni wazao wa Haruni,+ wenye wametakaswa. Toka patakatifu, kwa maana umetenda kwa kukosa uaminifu na hautapokea utukufu wowote kutoka kwa Yehova Mungu kwa sababu ya jambo hili.”
-