Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 20:6
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 6 Basi Mungu wa kweli akamuambia katika ndoto: “Ninajua kwamba ulifanya vile kwa moyo muzuri, kwa hiyo nilikuzuia usinitendee zambi. Ndiyo sababu sikukuruhusu umuguse.

  • Kumbukumbu la Torati 17:12
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 12 Mutu mwenye anatenda kwa kimbelembele kwa kukosa kumusikiliza kuhani mwenye anamutumikia Yehova Mungu wako ao kwa kukosa kumusikiliza muamuzi anapaswa kufa.+ Unapaswa kuondoa mambo ya mubaya katika Israeli.+

  • 1 Samweli 15:23
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 23 kwa maana uasi+ ni sawa na zambi ya uaguzi,+ na kuenda mbele kwa kimbelembele ni sawa na kutumia nguvu za uchawi na ibada ya sanamu.* Kwa sababu umekataa neno la Yehova,+ yeye pia amekukataa usikuwe mufalme.”+

  • 2 Samweli 6:7
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 7 Halafu kasirani ya Yehova ikawaka juu ya Uza, na Mungu wa kweli akamupiga na kumuua+ pale kwa sababu ya tendo lake la kukosa heshima,+ na akakufia pale karibu na Sanduku la Mungu wa kweli.

  • 2 Mambo ya Nyakati 26:16-18
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 16 Hata hivyo, wakati tu alikuwa na nguvu, moyo wake ukakuwa na majivuno na kufikia kuleta uharibifu wake mwenyewe, na alitenda kwa kukosa uaminifu kumuelekea Yehova Mungu wake kwa kuingia katika hekalu la Yehova ili kuchoma uvumba kwenye mazabahu ya uvumba.+ 17 Mara moja Azaria kuhani na makuhani wengine makumi munane (80) wa Yehova wenye uhodari wakamufuata ndani. 18 Wakapambana na Mufalme Uzia na kumuambia: “Haiko kazi yako, Uzia, kumuchomea Yehova uvumba!+ Ni makuhani tu ndio wanapaswa kuchoma uvumba, kwa maana wao ni wazao wa Haruni,+ wenye wametakaswa. Toka patakatifu, kwa maana umetenda kwa kukosa uaminifu na hautapokea utukufu wowote kutoka kwa Yehova Mungu kwa sababu ya jambo hili.”

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine