-
2 Wafalme 5:20-22Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
20 Gehazi+ mutumishi wa Elisha mutu wa Mungu wa kweli+ akasema katika moyo wake: ‘Angalia, bwana wangu ameachilia huyu Musiria Naamani+ kwa kukataa kupokea vitu vyenye alileta. Kama vile hakika Yehova anaishi, nitakimbia na kumufuata na nitakamata kitu fulani kutoka kwake.’ 21 Kwa hiyo Gehazi akafuata mbio Naamani. Wakati Naamani alimuona mutu fulani akimufuata akiwa anakimbia, akashuka kutoka kwenye gari lake ili akutane naye na akasema: “Je, mambo yote ni sawa?” 22 Halafu akasema: “Mambo yote ni sawa. Bwana wangu amenituma, akisema, ‘Angalia! Sasa hivi vijana wawili kutoka eneo lenye milima la Efraimu kutoka kwa wana wa manabii wamekuja kwangu. Tafazali, uwapatie talanta moja ya feza na nguo mbili za kubadilisha.’”+
-