42 Angalia! Mutumishi wangu,+ mwenye ninategemeza!
Muchaguliwa wangu,+ mwenye nimekubali!+
Nimeweka roho yangu ndani yake;+
Ataletea mataifa haki.+
2 Hatalalamika wala kupandisha sauti yake,
Na hatafanya sauti yake isikike katika barabara.+
3 Hatavunja utete wenye kupondekana,
Na hatazima utambi wenye kutoa moshi.+
Ataleta haki kwa njia ya uaminifu.+
4 Hatafifia wala kupondwa mupaka wakati ataweka haki katika dunia;+
Na visiwa vitaendelea kungojea sheria yake.