-
Marko 10:41-45Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
41 Wakati wale wengine kumi (10) walisikia jambo hilo, wakamukasirikia Yakobo na Yohana.+ 42 Lakini Yesu, akawaita na kuwaambia: “Munajua kwamba wale wenye wanaonekana kuwa wanatawala* mataifa wanapiga ubwana juu yao na wakubwa wao wanatumia mamlaka juu yao.+ 43 Haipaswe kuwa vile kati yenu; lakini kila mutu mwenye anataka kuwa mukubwa katikati yenu anapaswa kuwa mutumishi wenu,+ 44 na kila mutu mwenye anataka kuwa wa kwanza katikati yenu anapaswa kuwa mutumwa wa wote. 45 Kwa maana hata Mwana wa binadamu hakukuja ili watu wamutumikie, lakini ili yeye atumikie wengine+ na atoe uzima wake* kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi.”+
-