Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Matayo 9:27
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 27 Wakati Yesu alikuwa anatoka kule, wanaume wawili vipofu+ wakamufuata, wakisema kwa sauti kubwa: “Utusikilie huruma, Mwana wa Daudi.”

  • Marko 10:46-52
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 46 Kisha wakaingia Yeriko. Lakini wakati yeye na wanafunzi wake na watu wengi sana walikuwa wanatoka Yeriko, Bartimayo (mwana wa Timayo), kipofu mwenye kuomba-omba, alikuwa amekaa pembeni ya barabara.+ 47 Wakati alisikia kwamba ni Yesu Munazareti, akaanza kuita kwa sauti kubwa na kusema: “Mwana wa Daudi,+ Yesu, unisikilie huruma!”+ 48 Halafu watu wengi wakaanza kumukemea, wakimuambia anyamaze, lakini akaendelea kusema kwa sauti kubwa: “Mwana wa Daudi, unisikilie huruma!” 49 Kwa hiyo Yesu akasimama na kusema: “Mumuite akuje.” Basi wakamuita ule kipofu, wakamuambia: “Usiogope! Simama; anakuita.” 50 Akatupa nguo yake ya inje, akasimama haraka na kumuendea Yesu. 51 Kisha Yesu akamuuliza: “Unataka nikufanyie nini?” Ule kipofu akamuambia: “Raboni,* naomba niweze kuona tena.” 52 Na Yesu akamuambia: “Uende. Imani yako imekuponyesha.”+ Na mara moja akaanza kuona tena,+ na akaanza kumufuata katika barabara.

  • Luka 18:35-43
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 35 Sasa wakati Yesu alikaribia Yeriko, kipofu mumoja alikuwa amekaa pembeni ya barabara akiomba-omba.+ 36 Kwa kuwa alisikia watu wengi wakipita, akaanza kuuliza kama kuko nini. 37 Wakamuambia: “Ni Yesu Munazareti ndiye anapita!” 38 Basi akasema kwa sauti kubwa: “Yesu, Mwana wa Daudi, unisikilie huruma!” 39 Na wale wenye walikuwa mbele wakaanza kumukemea wakimuambia anyamaze, lakini akaendelea kusema kwa sauti kubwa: “Mwana wa Daudi, unisikilie huruma!” 40 Kisha Yesu akasimama na kuamuru wamuletee ule mutu. Wakati alikaribia, Yesu akamuuliza: 41 “Unataka nikufanyie nini?” Akasema: “Bwana, ninaomba niweze kuona tena.” 42 Basi Yesu akamuambia: “Ona tena; imani yako imekuponyesha.”+ 43 Na mara moja akaanza kuona tena, na akaanza kumufuata+ akimutukuza Mungu. Pia, wakati watu wote waliona jambo hilo, wakamusifu Mungu.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine