-
Marko 10:46-52Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
46 Kisha wakaingia Yeriko. Lakini wakati yeye na wanafunzi wake na watu wengi sana walikuwa wanatoka Yeriko, Bartimayo (mwana wa Timayo), kipofu mwenye kuomba-omba, alikuwa amekaa pembeni ya barabara.+ 47 Wakati alisikia kwamba ni Yesu Munazareti, akaanza kuita kwa sauti kubwa na kusema: “Mwana wa Daudi,+ Yesu, unisikilie huruma!”+ 48 Halafu watu wengi wakaanza kumukemea, wakimuambia anyamaze, lakini akaendelea kusema kwa sauti kubwa: “Mwana wa Daudi, unisikilie huruma!” 49 Kwa hiyo Yesu akasimama na kusema: “Mumuite akuje.” Basi wakamuita ule kipofu, wakamuambia: “Usiogope! Simama; anakuita.” 50 Akatupa nguo yake ya inje, akasimama haraka na kumuendea Yesu. 51 Kisha Yesu akamuuliza: “Unataka nikufanyie nini?” Ule kipofu akamuambia: “Raboni,* naomba niweze kuona tena.” 52 Na Yesu akamuambia: “Uende. Imani yako imekuponyesha.”+ Na mara moja akaanza kuona tena,+ na akaanza kumufuata katika barabara.
-
-
Luka 18:35-43Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
35 Sasa wakati Yesu alikaribia Yeriko, kipofu mumoja alikuwa amekaa pembeni ya barabara akiomba-omba.+ 36 Kwa kuwa alisikia watu wengi wakipita, akaanza kuuliza kama kuko nini. 37 Wakamuambia: “Ni Yesu Munazareti ndiye anapita!” 38 Basi akasema kwa sauti kubwa: “Yesu, Mwana wa Daudi, unisikilie huruma!” 39 Na wale wenye walikuwa mbele wakaanza kumukemea wakimuambia anyamaze, lakini akaendelea kusema kwa sauti kubwa: “Mwana wa Daudi, unisikilie huruma!” 40 Kisha Yesu akasimama na kuamuru wamuletee ule mutu. Wakati alikaribia, Yesu akamuuliza: 41 “Unataka nikufanyie nini?” Akasema: “Bwana, ninaomba niweze kuona tena.” 42 Basi Yesu akamuambia: “Ona tena; imani yako imekuponyesha.”+ 43 Na mara moja akaanza kuona tena, na akaanza kumufuata+ akimutukuza Mungu. Pia, wakati watu wote waliona jambo hilo, wakamusifu Mungu.+
-