-
Matayo 4:1-10Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
4 Kisha Yesu akaongozwa na roho kuenda katika jangwa ili ajaribiwe+ na Ibilisi.+ 2 Kisha kufunga kwa siku makumi ine (40) muchana na usiku, akasikia njaa. 3 Na Mujaribu+ akakaribia na kumuambia: “Kama wewe uko mwana wa Mungu, ambia majiwe haya yakuwe mikate.” 4 Lakini akajibu: “Imeandikwa: ‘Mwanadamu hapaswe kuishi kwa mukate tu, lakini kwa kila neno lenye linatoka katika kinywa cha Yehova.’”*+
5 Kisha Ibilisi akamupeleka katika ule muji mutakatifu,+ na akamusimamisha juu ya munara wa* hekalu+ 6 na kumuambia: “Kama wewe ni mwana wa Mungu, ujitupe chini, kwa sababu imeandikwa: ‘Ataamuru malaika wake kwa ajili yako,’ na, ‘Watakubeba katika mikono yao, ili usigonge muguu wako kwenye jiwe.’”+ 7 Yesu akamuambia: “Tena imeandikwa: ‘Haupaswe kumujaribu Yehova* Mungu wako.’”+
8 Tena Ibilisi akamupeleka kwenye mulima wenye kuwa na urefu wenye hauko wa kawaida na kumuonyesha falme zote za ulimwengu na utukufu wa falme hizo.+ 9 Na akamuambia: “Nitakupatia vitu hivi vyote ukianguka chini na kunifanyia tendo la ibada.” 10 Basi Yesu akamuambia: “Toka mbele yangu, Shetani! Kwa sababu imeandikwa: ‘Yehova* Mungu wako ndiye unapaswa kuabudu,+ na yeye peke yake ndiye unapaswa kutolea utumishi mutakatifu.’”+
-
-
Luka 4:1-13Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
4 Basi Yesu, akiwa amejaa roho takatifu, akaondoka kutoka Yordani, na akaongozwa na roho huku na huku katika jangwa+ 2 kwa siku makumi ine (40), akijaribiwa na Ibilisi.+ Na hakukula kitu chochote katika siku hizo, kwa hiyo, wakati ziliisha, akasikia njaa. 3 Halafu Ibilisi akamuambia: “Kama wewe ni mwana wa Mungu, ambia jiwe hili likuwe mukate.” 4 Lakini Yesu akamujibu: “Imeandikwa, ‘Mwanadamu hapaswe kuishi kwa mukate tu.’”+
5 Basi akamupeleka juu kwenye mulima na kumuonyesha mara moja falme zote za dunia yenye kuikaliwa na watu.+ 6 Kisha Ibilisi akamuambia: “Nitakupatia mamlaka yote hii na utukufu wake, kwa sababu nimeipewa,+ na ninaipatia mutu yeyote mwenye ninataka. 7 Kwa hiyo, kama unafanya tendo moja la ibada mbele yangu, yote itakuwa yako.” 8 Yesu akajibu na kumuambia: “Imeandikwa, ‘Yehova* Mungu wako ndiye unapaswa kuabudu, na yeye peke yake ndiye unapaswa kutolea utumishi mutakatifu.’”+
9 Kisha akamupeleka Yerusalemu, akamusimamisha juu ya munara wa* hekalu na kumuambia: “Kama wewe ni mwana wa Mungu, ujitupe chini kutoka hapa,+ 10 kwa maana imeandikwa, ‘Ataamuru malaika wake kwa ajili yako, ili wakulinde,’ 11 na, ‘Watakubeba katika mikono yao, ili usigonge muguu wako kwenye jiwe.’”+ 12 Yesu akamujibu na kumuambia: “Imeandikwa, ‘Haupaswe kumujaribu Yehova* Mungu wako.’”+ 13 Kwa hiyo Ibilisi, wakati alimaliza majaribu yote, akamuacha mupaka wakati mwingine wenye kufaa.+
-