-
Matayo 14:3-5Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
3 Herode* alikuwa amemukamata Yohana, akamufunga na kumutia katika gereza kwa sababu ya Herodia, bibi ya Filipo ndugu yake.+ 4 Kwa maana Yohana alikuwa anamuambia Herode: “Hauruhusiwe kuwa na mwanamuke huyo.”+ 5 Lakini, hata kama Herode alitaka kumuua, aliogopa watu, kwa sababu walimuona Yohana kuwa nabii.+
-
-
Marko 6:17-20Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
17 Kwa maana Herode mwenyewe alikuwa ametuma watu wamukamate Yohana, akamufunga katika gereza kwa sababu ya Herodia, bibi ya Filipo ndugu yake, kwa kuwa Herode alikuwa amemuoa.+ 18 Kwa maana Yohana alikuwa anamuambia Herode: “Hauruhusiwe kuwa na bibi ya ndugu yako.”+ 19 Basi Herodia alimuwekea Yohana kinyongo* na alitaka kumuua, lakini hakuweza. 20 Kwa maana Herode alikuwa anaogopa Yohana, na alimujua kuwa mwenye haki na mutakatifu,+ na alikuwa anamulinda. Kisha kumusikiliza, alikosa kabisa afanye nini, lakini aliendelea kumusikiliza kwa furaha.
-