-
Matendo 2:29-32Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
29 “Wanaume, ndugu zangu, inaruhusiwa kusema na ninyi kwa uhuru wa kusema juu ya Daudi, kichwa cha familia, kwamba alikufa na akazikwa,+ na kaburi lake liko hapa mupaka leo. 30 Kwa sababu alikuwa nabii na alijua kwamba Mungu alikuwa amemuapia kwa kiapo kwamba ataikalisha mumoja kati ya wazao wake* kwenye kiti chake cha ufalme,+ 31 aliona mbele ya wakati na alisema juu ya ufufuo wa Kristo, kwamba hakuachwa katika Kaburi* na mwili wake haukuona uharibifu.*+ 32 Mungu alimufufua huyu Yesu, na sisi wote tuko mashahidi wa jambo hilo.+
-