Ezekieli
5 “Sasa wewe, mwana wa binadamu, kamata upanga mukali ili uutumie kama wembe wa mukata-nywele. Nyoa kichwa chako na ndevu zako, na ukamate mizani* za kupimia na ugawanye nywele hizo katika mafungu. 2 Utateketeza sehemu moja ya tatu (1/3) ya nywele hizo katika moto ndani ya muji wakati siku za kuzunguka kwa ajili ya vita zitamalizika.+ Kisha utakamata ingine sehemu moja ya tatu na utaipiga kwa upanga kuzunguka muji* pande zote,+ na sehemu moja ya tatu ya mwisho utaisambaza kwenye upepo, na nitachomoa upanga ili kuwafuatilia.+
3 “Pia unapaswa kukamata nywele kidogo na kuzifunga katika mikunjo ya* nguo yako. 4 Na zingine utazikamata na kuzitupa katika moto na kuziteketeza. Moto utatoka mule na kuenea katika nyumba yote ya Israeli.+
5 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Huyu ni Yerusalemu. Nimemutia katikati ya mataifa, na inchi zinamuzunguka pande zote. 6 Lakini ameasi maamuzi yangu ya hukumu na sheria zangu, akitenda uovu zaidi kuliko mataifa na inchi zenye kumuzunguka pande zote.+ Kwa maana wamekataa maamuzi yangu ya hukumu, na hawakutembea katika sheria zangu.’
7 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Kwa sababu mulikuwa watu wenye kuleta muvurugo zaidi kuliko mataifa yote yenye kuwazunguka pande zote na hamukutembea katika sheria zangu wala kushika maamuzi yangu ya hukumu lakini, kuliko kufanya vile, mulifuata maamuzi ya hukumu ya mataifa yenye kuwazunguka pande zote,+ 8 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Angalia, nitapigana na wewe, Ee muji,+ na mimi mwenyewe nitaleta hukumu katikati yako mbele ya macho ya mataifa.+ 9 Nitafanya ndani yako mambo yenye sijapata kufanya mbele, na yenye sitafanya tena, kwa sababu ya mazoea yako yote yenye kuchukiza.+
10 “‘“Kwa hiyo baba wenye kuwa kati yenu watakula wana wao,+ na wana watakula baba zao, na nitaleta hukumu kati yenu na kuwasambaza kila upande* wale wote wenye walibakia katikati yenu.”’+
11 “‘Kwa hiyo, kama vile hakika ninaishi,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema, ‘kwa sababu ni patakatifu pangu ndipo mulichafua kwa sanamu zenu zote zenye kuchukiza na mazoea yenu yote yenye kuchukiza,+ mimi pia nitawakataa;* jicho langu halitasikitika, na sitakuwa na huruma yoyote.+ 12 Sehemu yako moja ya tatu (1/3) watakufa kwa ugonjwa wa kuambukiza ao wataangamia kwa njaa katikati yako. Sehemu ingine moja ya tatu wataanguka kwa upanga kukuzunguka pande zote.+ Na nitasambaza sehemu moja ya tatu ya mwisho katika kila upande,* na nitachomoa upanga ili kuwafuatilia.+ 13 Halafu hasira yangu itafika mwisho, na kasirani yangu kali juu yao itatulia, na nitatosheka.+ Nao watalazimika kujua kwamba mimi, Yehova, nimesema kwa kukazia kwamba watu washikamane na mimi tu,+ wakati nitamaliza kumwanga kasirani yangu kali juu yao.
14 “‘Nitakufanya kuwa mahali kwenye kumeharibiwa na kitu cha haya kati ya mataifa yenye kukuzunguka na mbele ya macho ya kila mupita-njia.+ 15 Utakuwa kitu cha haya na kuzarauliwa,+ mufano wa kuonya na kitu cha kuogopesha sana kwa mataifa yenye kukuzunguka, wakati nitaleta hukumu juu yako kwa hasira na kasirani kali na kwa azabu yenye kasirani kali. Mimi, Yehova, nimesema.
16 “‘Nitatuma juu yao ile mishale hatari yenye kuleta njaa ili kuwaharibu. Mishale yenye nitatuma itawaharibu ninyi.+ Nitafanya njaa ikuwe mubaya zaidi kwenu kwa kuondoa akiba yenu ya chakula.*+ 17 Nitatuma juu yenu njaa na wanyama wa pori wakali,+ nao watafanya mukose watoto. Ugonjwa wa kuambukiza na umwangaji wa damu vitawalemea, na nitaleta upanga juu yenu.+ Mimi, Yehova, nimesema.’”